quinta-feira, 26 de fevereiro de 2015

GHARIKA NA JANGWA


Kutafakari kutoka Mwanzo 9: 8-15; 1Pt 3: 18-22; Mk 1: 12-15

Tumeanza safari yetu ya toba inayoitwa Kwaresima. Kipindi hiki kinapendekeza safari ya ubadilifu, kutuandaa kuadhimisha mafumbo makuu ya imani yetu, kufanya upya ahadi yetu na maisha mapya kutokana na Kristo na ufufuo wake. Msimu wa Kwaresima ni mafungo makubwa ya muda wa siku arobaini kwa Wakristo wengi, kutukumbusha kuhusu muda wa siku arobaini ya Musa juu ya Mlima Sinai ili kuzipokea Amri na miaka arobaini ya safari ya usafishaji wa watu wa Israeli katika jangwa na uzoefu wa Yesu katika jangwa pia kabla ya kazi yake. Yesu alishinda majaribu yote  kwa sababu akajiruhusu kuongozwa na Roho Mtakatifu. Kila mtu ambaye anazifuata nyayo zake, na aliyefunguliwa kwa safari ya ubadilifu, yeye husaidiwa na nguvu kutoka juu ili kufanya mapenzi ya Mungu kwa mafanikio.

Masomo ya Jumapili hii yanatuingiza katika safari ya upya wa ubatizo wetu, kutuonyesha njia iliyopendekezwa na Mungu ili kufanya maisha mapya duniani. Kupitia Nuhu na familia yake Mungu anafanya agano la kwanza na ubinadamu, kufanya upya uumbaji wote. Pendekezo hapa ni uumbaji upya, ambao hutokea wakati mwanadamu hubadilisha chaguzi zake, kufanya uhusiano mpya na Mungu na viumbe vyingine vyote vilivyo hai. Agano ni ishara kwamba Mungu hataki kupoteza binadamu, kupendekeza daima nafasi mpya ya utakaso na ubadilifu. Katika somo la pili, Mtakatifu Petro anaongea kuhusu athari ya gharika kwa uumbaji wote kama ishara ya ubatizo ambao humtakasa, kumpa binadamu maisha mapya katika Kristo.

Katika sehemu ya kwanza ya injili, Yesu anaongozwa jangwani kwa nguvu ya Roho. Kama hii alihamasishwa sana kuishi uzoefu huu kulenga katika maandalizi ya kazi iliyokabidhiwa na Baba. Katika Biblia, Jangwa ni mahali pazuri daima kukutana na Mungu na palikuwa ni mahali pale ambapo Watu wa Israeli walihisi upendo na ulinzi ya Mungu mara kwa mara. Kwa Yesu uzoefu huo ulikuwa wa maana na Kupitia huo aliweza kutambua bora mpango wa Mungu. Wakati huu pia alijaribiwa na Shetani na aliyashinda majaribu yote kwa kuwa mtiifu kwa Baba yake. Alikubali hali hiyo ili kuonyesha jinsi ya kushinda mtego wa mshawishi. Majaribu ya mali, nguvu na utukufu yaliyokabiliwa na Yesu hayakumvuruga kutoka kufanya mapenzi ya Mungu.

Katika sehemu ya pili ya injili tuna muhtasari wa mwanzo wa kazi ya Yesu na tangazo la Ufalme wa Mungu na mwaliko kwa ubadilifu. Uwepo wa Yesu unaleta Ufalme wa Mungu, kuanzisha wakati mpya, wakati wa wokovu. Hiyo ni habari njema ambayo ilitarajiwa kwa wote. Ili kuamini habari njema iliyotangazwa na Yesu, ubadilifu ni muhimu. Moyo ni kitovu cha maamuzi na ubadilifu unatokea moyoni, kwa hivyo imani ya kweli katika Yesu inawezekana kama moyo unabadilishwa.

Katika uzoefu wake jangwani, Yesu aliongozwa na Roho, akasaidiwa na Malaika na akawa makini sana kuhusu mpango wa Mungu. Kwa hivyo hakuna kilichomvuruga kutoka muhimu zaidi. Kama wafuasi wa Yesu, mara kwa mara sisi hushawishiwa kuacha kwa sababu ni mpango wa mshawishi. Lakini mfano wa uaminifu wa Mwalimu Yesu ni mwaliko kwetu tujiruhusu kuongozwa na Roho Mtakatifu, kusaidiwa na wengine na kuwa na malengo ya wazi sana maishani mwetu ili kutambua vizuri katika kila kitu. Majaribu zaidi ya kawaida katika jumuiya zetu ni kufikiri kwamba kuna watu wa kutosha kutumikia au kutumia baadhi ya majukumo ili kutawala na kuwafedhehesha wengine. Kwaresima hii itusaidie katika safari yetu ya ubadilifu, kutuhamasisha kukaa kwa umakini katika muhimu zaidi - kama Yesu kuhusu mpango wa Mungu - ili kushinda majaribu kufuata njia zingine.

Fr. Ndega

Mapitio: Mwalimu Patrick

Nenhum comentário: