sábado, 30 de junho de 2018

YESU ANAWEZA KUURUDISHA UZIMA KWA SABABU YA IMANI



Kutafakari kutoka Hek 1,13-15;2,23-24; Mk 5, 21-43


Mauti yako duniani lakini hayatoki kwa Mungu kwa sababu yeye ndiye uzima na kutuumba kwa uzima. Mungu hataki mauti ya watoto wake lakini hazuii watende dhidi ya mapenzi yake kwa sababu anaheshimu uhuru wao wa uamuzi. Huu ndio ujumbe wa kifungu cha Kitabu cha Hekima. Andiko hili linachukua tena tukio la uumbaji na kuonyesha nia ya Mungu alipoumba viumbe vyote. Ingawa ndiye binadamu anayefanyika kwa mfano na kwa sura ya Mungu, viumbe vingine pia vinaonyesha uzuri wa nafsi ya Mungu na kuongelea yeye. Hivyo, binadamu anaitwa kuishi kwa maelewano na viumbe vyote kwa sababu yeye na vingine vina asili sawa. Mambo yote binadamu anayepanga kufanya kwa ajili ya viumbe vingine yanaleta matokeo kwa maisha yake mwenyewe.    
Baada ya kufukuza pepo wachafu kutoka mtu fulani, Yesu aliendelea anahubiri habari njema na kutenda mambo mema mengi. Watu wakastaajabu. Kweli Yesu alikuwa mtu maarufu na mahali popote ambapo alifika mara makutano makuu yalikusanika yakimsongasonga ili kusikiliza neno la Mungu. Kulingana na andiko la leo Yesu alivuka ziwa la Galilaya na kubaki kando ya bahari. Tena umati wa watu ulikusanika kumsikiliza. Kwa upande wa Yesu, yeye alipatikana kwa ajili ya kujifunza watu na kuwasaidia katika mahitaji yao. Kwa upande wa watu, imani ndiyo kipengele msingi.
Alipozungumza, mtu mmoja aliye mkuu wa sinagoga aliyeitwa Yairo alimwendea kumwomba aponye binti yake aliyekuwa mgonjwa na mara Yesu alienda pamoja naye na wanafunzi watatu. Lakini wakati wa safari mtoto alikufa. Yesu alimwambia Yairo: “uwe na imani tu!” kweli, kwa sababu ya imani ya Yairo na mke wake mtoto alifufuliwa. Kabla ya Yesu kwenda kwenye nyumba ya Yairo, mkutano mkuu waliomfuata wakisongasonga. Miongoni mwao alikuwako mwanamke fulani aliyekuwa mgonjwa wa kutoka damu. Yeye alimgusa Yesu kwa imani kubwa na mara akapata kuponywa. Yesu alimwambia: “binti, imani yako imekuokoa”.
Katika matukio hayo mawili ndiyo imani kipengele cha msingi ili Yesu atende muujiza. “Imani ndiyo msingi, kama Marko asemavyo kwamba, Yesu hakuweza kufanya miujiza Nazareti kwa sababu watu walikosa imani (Mk 6, 1-6).” Miujiza siyo uchawi ili mtu aseme: “utuonyeshe kitu nasi tutasadiki!”, bali ni mwaliko wa kutusaidia kuzikuza imani yetu. Katika miujiza mingi ya Yesu, imani ndicho kipengele cha msingi. “Hata iwapo siyo imani kutoka kwa mgonjwa mwenyewe moja kwa moja, kwa mfano binti Yairo, imani ya jumuiya ni muhimu (Mk 2,5).” Tukumbuke tena wakati Yesu alipokuwa ndani ya nyumba fulani iliyojaa watu. Kikundi kimoja cha watu ambacho kilimbeba mtu mgonjwa, kilifanya shimo katika dari ya nyumba na kupata kumuweka mtu mgonjwa mbele ya Yesu. Kwa sababu ya imani yao, Yesu alimponya mtu mgonjwa. 
Ndilo jambo la ajabu inayoonekana katika matukio mawili, yaani mwanamke fulani alikuwa mgonjwa kwa miaka kumi na miwili na mtoto alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili. Nambari hii yaani kumi na miwili ndiyo ishara muhimu katika biblia na kumaanisha Watu wa Israeli na ubinadamu mzima. Wote yaani mwanamke na mtoto wanahitaji uzima kwa sababu ya ugonjwa. Ndiye Yesu peke yake anayeweza kuwapatia uzima kwa kuwa yeye mwenyewe ndiye uzima wa milele. “Mwanamke mgonjwa wa kutokwa damu, alikuwa na imani iliyosukuma amguse Yesu na hivyo akaweza kuponywa.”  Kulingana na Agano la Kale, kugusa mavazi ni kugusa mtu mwenyewe. Tukumbuke kwamba ilitosha kupata mavazi ya Elijah ili Elisha apokee roho yake. “Tendo la kugusa ni ishara ya upendo, kama vile mtu anapomgusa mgonjwa, ni ishara kwamba anampenda na kumjali katika hali yake yote.” Ingawa hali ya mwanamke ilikuwa uchafu na yeyote aliyekutana naye alikuwa mchafu, Yesu aliruhusu kuguswa naye na kubadilisha hali iliyotarajiwa na wote, yaani badala ya kuwa mchafu yeye alisababisha usafi mwilini mwa mwanamke.
 “Usiogope; amini tu...” yalikuwa maneno ya Yesu kwa Yairo alimpoteza mtoto wake. Maneno ya Yesu ni maonyesho ya upendo na huruma yake kwa ajili ya walioteseka. Tumejifunza na kuhisi kwamba “moyo wa Yesu ni chemchemi ya huruma” na Maandiko yenyewe yashuhudia kwamba “Kwa upande wake tumepokea neema juu ya neema”. Habari hii inaiimarisha imani yetu na kulifufua tumaini letu. Nasi kama Yairo na watu wengine twapewa changamoto ya kuamini kuwa Yesu anaweza kurudisha  uzima. Kilichotokea katika maisha ya Yesu kilikuwa kimelenga katika kuwaelimisha wale wenye imani kuwa wao pia watapata uzima kwa sababu, kulingana na mapenzi ya Mungu maisha yetu yanafaa kupata ukamilifu kwa kufufuka kama Mwanawe. Uzima kwa mwenye imani wawezekana kutokana na ufufuko wa Kristo. Tujaribu kumwamini Kristo na matendo yetu yawe tangazo la uzima uliomo ndani yetu ambao yeye mwenyewe anatuhakikishia. 

Fr Ndega

segunda-feira, 25 de junho de 2018

A VOCAÇÃO COMO PROCLAMAÇÃO DA MISERICÓRDIA E PROXIMIDADE DE DEUS



Reflexão a partir de Is 49, 1-6; At 13, 22-26; Lc 1, 57-66.80

        Somos convidados a celebrar a solenidade do Nascimento de São João Batista. Com exceção de Nossa Senhora, este é o único Santo do qual celebramos também o nascimento. Isto é devido a sua estreita relação com a vinda do Filho de Deus ao mundo. A gestação do plano salvífico de Deus não se dá nas grandes estruturas (Templo, Palácio de Herodes, etc.) nem nos grandes eventos, mas na vida cotidiana de pessoas simples, atentas e abertas às surpresas de Deus. É, portanto, através do ventre de duas mulheres, Maria e de Isabel, que Deus quis tornar visível a sua presença misericordiosa no mundo.

       O trecho da primeira leitura é o Segundo Canto do Servo, do profeta Isaías. E segundo este cântico, é Deus mesmo que plasma o seu servo desde o ventre materno e lhe confia uma missão que não se limita a um pequeno grupo ou aos limites de um determinado país. É da vontade de Deus que seu servo seja luz para iluminar os povos a fim de que a sua salvação chegue a todos. Motivado pela certeza da presença de Deus em sua vida, este servo decide investir todas as suas forças pela causa daquele que o chamou. Este servo nos ajuda a refletir a vocação como uma iniciativa divina, um dom que a pessoa recebe não para si mesmo, mas para o bem dos outros. Aquele que nos chamou se faz próximo de nós para que nossas escolhas correspondam às suas expectativas sobre nossas vidas.

       De acordo com a segunda leitura, Deus enviou Jesus como Salvador. Sua vinda foi preparada por João através de um batismo de conversão para preparar a Deus um povo bem-disposto. Quando João é interrogado sobre sua missão, ele não recorre a títulos ou privilégios, o que colocaria sua própria pessoa no centro, mas responde em subtração: “Eu não sou”, “eu não sou digno”. “Eu não sou!” contrasta com “Eu sou!”, que é o próprio nome de Deus. Aqui está enraizada a verdadeira grandeza do ser humano: ao reconhecer que Deus é Deus, aquele que é verdadeiramente, enquanto nós não existimos por nós mesmos, mas apenas em estreita dependência do Criador. A vida e as atitudes de João nos ajudam a sermos conscientes de nossa identidade para não pretendermos ocupar na vida das pessoas o lugar que pertence só a Deus.

      O evangelho fala do nascimento de João Batista como uma grande ação da misericórdia de Deus na vida de Isabel, considerada infeliz e castigada por causa de sua esterilidade.  Agora ela experimenta uma nova vida. Assim diz o texto: “os vizinhos e parentes ficaram sabendo que o senhor tinha manifestado nela a sua grande misericórdia, e se alegraram com ela. Aqui temos dois aspectos importantes a considerar: primeiro, a revelação da misericórdia de Deus é um evento que não segue os critérios humanos; segundo, traz alegria intensa à vida das pessoas envolvidas e aos que delas se aproximam. Diante disso, o sacerdote é silenciado, enquanto à mulher é dada a oportunidade de proclamar: “ele será chamado João”. João significa “dom de Deus”. Somente a pessoa que faz a experiência de ser dom é capaz reconhecer a vida, o nascimento de uma criança como um dom de Deus. Em seguida, ajudado em sua fé, também o sacerdote Zacarias abre a sua boca para proclamar a proximidade e fidelidade de Deus na história do seu povo. E o que será este menino? Será o grande precursor. Entre os nascidos de mulher, ninguém é tão grande quanto ele.

       O nascimento de João é pré-anúncio do nascimento do Salvador e a sua missão é preparar o caminho para o Filho de Deus encarnado. De fato, o anúncio da boa notícia que Jesus traz começa propriamente com a atividade deste precursor, considerado “o maior de todos os profetas”. João é uma ponte entre o antigo e o novo testamento. “A passagem entre os dois testamentos é um tempo de silêncio: a palavra, tirada do templo e do sacerdócio, está sendo tecida no ventre de duas mães. Deus traça a sua história sobre o calendário da vida, e não no estreito limite das instituições”.

      Antes de iniciar sua missão, João viveu na solidão do deserto, totalmente aberto à inspiração divina. No deserto, a partir da experiência da Palavra de Deus, ele aprendeu a ser testemunha da verdade. Nos causa admiração o seu estilo de vida simples, especialmente seu modo de vestir-se e a sua comida. A grandeza de João foi demonstrada em reconhecer a grandeza do Senhor, considerando-se como apenas uma voz que grita “do” deserto preparando o caminho para aquele que deve vir. Em sua mensagem, João proclamava a misericórdia de Deus e além das palavras, ele batizava as pessoas como um sinal concreto de conversão e abertura a esta misericórdia. A razão da credibilidade da mensagem de João não eram apenas suas palavras, mas também o seu estilo simples e humilde de viver, isto é, a sua coerência de vida. Mesmo que não existissem as palavras, a sua vida era já uma proclamação concreta da nova realidade que Jesus trouxe à terra.

      A vida de João nos diz que também nós podemos fazer a diferença na vida de muitas pessoas, mas não existe profecia sem “experiência de deserto”, isto é, sem uma relação de intimidade com Deus e com sua Palavra. É, portanto, a partir do “deserto” que nos vem a proposta de voltar, de mudar os caminhos, a mentalidade, em suma, de mudar alguma coisa ou tudo. Se a nossa vida for transformada a partir da Palavra seremos realmente testemunhas de uma nova realidade, de boas notícias, porque o testemunho de vida é mais eficaz do que as palavras. “A missão de João nos ensina sobre o fato de que também nós devemos preparar o coração para acolher o Senhor e se queremos conhecê-lo e segui-lo mais de perto, devemos arar o terreno da nossa interioridade”. Que possamos, a partir do exemplo de João Batista, viver a nossa vocação como proclamação da misericórdia e proximidade de Deus.

Fr Ndega



domingo, 24 de junho de 2018

LA VOCAZIONE COME PROCLAMAZIONE DELLA MISERICORDIA E VICINANZA DI DIO



Riflessione a partire di Is 49, 1-6; At 13, 22-26; Lc 1, 57-66.80


Siamo invitati a celebrare la solennità della natività di S Giovanni Battista. Insieme alla Madonna, questo è l’unico santo del quale si celebra anche la nascita. Questo è dovuto alla sua stretta relazione con la venuta del Figlio di Dio. La gestazione del piano salvifico di Dio non si dà nelle grandi strutture (tempio, palazzo, etc.) e grandi avvenimenti, ma nel quotidiano di persone semplici, abituate e aperte alle sorprese di Dio. La grande collaborazione ci viene data da Maria ed Elisabetta attraverso le quali Dio rende visibile la sua presenza misericordiosa nel mondo.
La prima lettura è tratta dal libro del profeta Isaia. Questo brano è conosciuto come il Secondo Cantico del Servo del Signore. Secondo questo cantico, è il proprio Dio che plasma il suo servo sin dal grembo materno e gli affida una missione che non si limita a un piccolo gruppo né ai confini di un determinato paese. È volontà di Dio che il suo servo diventi luce per illuminare le nazione affinché il suo progetto salvifico sia conosciuto da tutti. Motivato per la vicinanza di Dio accanto a sé, il servo decide di impegnare tutte le sue energie per la causa di Colui che lo ha chiamato. Questo servo ci aiuta a pensare alla vocazione come iniziativa divina, un dono che si riceve non per se stesso ma per il bene degli altri. Colui che ci ha chiamato ci è molto vicino perché le nostre scelte corrispondano alle sue aspettative sulla nostra vita.
La seconda lettura ci ricorda che Dio inviò Gesù come Salvatore. La sua venuta è stata preparata da Giovanni predicando un battesimo di conversione per preparare a Dio un popolo ben disposto. Quando Giovanni viene interrogato sulla sua missione egli non ricorre a titoli o a privilegi, a ciò che metterebbe al centro la sua persona, ma risponde: io non sono, io non sono degno. “’Non sono!” si contrappone a “Io sono!”, il nome proprio di Dio. Qui si radica la vera grandezza dell’uomo: nel riconoscere che Dio è Dio, Colui che solo “è”, mentre noi non esistimo per noi stessi, ma solo in stretta dipendenza dal Creatore. La vita e latteggiamento di Giovanni ci aiutano ad essere consapevoli della nostra identità per non pretendere di assumere nella vita degli altri il posto che appartiene solo a Dio.
Il vangelo parla della nascita di Giovanni Battista come una grande azione della misericordia di Dio nella vita di Elisabetta, considerata sfortunata a causa della sua sterilità.  Ora ha una nuova vita. Infatti, “I vicini e i parenti udirono che il Signore aveva manifestato in lei la sua grande misericordia, e si rallegravano con lei”. Abbiamo qui due aspetti a considerare: primo, la rivelazione della misericordia di Dio è un avvenimento che sfugge ai criteri umani, segue una logica diversa; secondo, porta intensa gioia alla vita delle persone coinvolte e alle altre che si avvicinano da loro. Davanti a questo il sacerdote tace e è dato alla donna l’opportunità di proclamare: “Egli si chiamerà Giovanni”. Giovanni vuol dire dono di Dio. Solo la persona che fa lesperienza di essere dono può riconoscere la vita, la nascita di un bambino come dono di Dio. Subito dopo questa testimonianza e, quindi, aiutato nella sua fede, il sacerdote Zaccaria apre la sua bocca per proclamare la vicinanza e fedeltà di Dio nella storia del suo popolo. E cosa sarà questo bambino? Egli sarà il grande precursore perché la mano del Signore era con lui.
La nascita di Giovanni è preannuncio della nascita del Salvatore e la sua missione è di preparare la via al Figlio di Dio incarnato. La buona notizia di Gesù inizia proprio con l’attività di questo precursore, chiamato ‘il maggiore dei profeti’. Giovanni è un ponte tra l’Antico e il Nuovo Testamento. “Il passaggio tra i due testamenti è un tempo di silenzio: la parola, tolta al tempio e al sacerdozio, si sta intessendo nel ventre di due madri. Dio traccia la sua storia sul calendario della vita, e non nel confine stretto delle istituzioni”.
Prima di iniziare la sua missione, Giovanni ha vissuto nella solitudine del deserto, totalmente aperto all’ispirazione di Dio. In quel luogo ha imparato dalla Parola di Dio come testimoniare la verità. Ci colpisce il suo stile di vita semplice, specialmente riguardo il vestito e il cibo. La grandezza di Giovanni era dimostrata nel riconoscere la grandezza del Signore, considerando se stesso come soltanto una voce che grida “dal” deserto preparando la strada a colui che deve venire. Nel suo messaggio, Giovanni proclamava la misericordia di Dio e oltre le parole, egli battezzava la gente come un segno concreto di conversione e apertura a questa misericordia di Dio. La ragione della credibilità del messaggio di Giovanni non erano solamente le sue parole, ma anche la sua umiltà e il suo stile semplice di vivere. Anche se le parole non ci fossero, la sua vita era già un vero annuncio della nuova realtà che Gesù ha portato sulla terra.
Giovanni ci dice che possiamo fare la differenza nella vita di molte persone, ma non c’è profezia senza ‘esperienza di deserto’, cioè, senza prendere sul serio un rapporto di vicinanza con Dio e con sua Parola. È, quindi, dal ‘deserto’ che ci viene la proposta di ritornare, di cambiare le vie, la mentalità, insomma, di cambiare qualcosa. Se la nostra vita è cambiata dalla Parola saremo davvero testimoni di una nuova realtà, di una buona notizia perché la testimonianza di vita è più efficace delle parole. “La missione di Giovanni ci istruisce circa il fatto che anche noi dobbiamo preparare il cuore ad accogliere il Signore e se vogliamo conoscerlo e seguirlo più da vicino dobbiamo arare il terreno della nostra interiorità”. A partire dall’esempio di Giovanni Battista, viviamo la nostra vocazione come proclamazione della misericordia e vicinanza di Dio.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

sábado, 16 de junho de 2018

UFALME WA MUNGU NDIO KAMA MBEGU



Kutafakari kuhusu  Ezekieli 17: 22-24; 2Wakorinto 5: 6-10; Marko 4: 26-34


         Kiini ya liturjia hii ni uwepo wa kimya na ufanisi wa ufalme wa Mungu miongoni mwetu. Mungu anafanya mambo yote kwa wema wetu na kutarajia tumwamini yeye kuliko nguvu zetu.

       Somo la kwanza linaongea kuhusu hali ya utumwa wa Babeli katika mwaka wa 597 K.K. na kumjulisha Ezekieli kama mmoja wa manabii aliyeandamana na watu wa Israeli katika kipindi hiki kigumu. Watu waliishi hali ya kuchanganyikiwa katika maisha yao bila matarajio ya mabadiliko. Lakini pamoja mwao alikuwako Ezekieli aliyewaimarisha kama mjumbe wa Mungu. Kulingana na nabii huyo, Mungu hakuwasahau; yeye yupo miongoni mwao na kuwaokoa, akiwaletea maisha mapya na kuwafanya kuwa rejeo kwa ajili ya kutangaza wema wake kwa mataifa yote. Katika mwendo huu wa ukombozi watu walinganishwa kama mmea mdogo utakaokuwa mti mkubwa. Basi, Mungu atachukua watu wake waliodhulumiwa na kuaibishwa, atawainua kama chombo cha wokovu wake. Njia hii ya Mungu ya kutenda inakumbukika katika wimbo wa Bikira Maria: “Bwana amewashusha wenye nguvu kutoka viti vyao vya enzi, na akawakweza wanyenyekevu”.

       Kulingana na Mtakatifu Paulo, sisi ni kama wageni, watu waliohamishwa ulimwenguni huu, mbali sana kutoka makao yetu. Sisi ni wa Mungu nasi hatuwezi kuridhishwa kwa ulimwengu huu, kwa sababu zawadi kuu ya imani ambayo tumepokea kutoka kwake inautoa mwelekeo kamili kwa maisha yetu ili tufikie marudio salama katika Mungu mwenyewe. Zawadi ya imani inatuimarisha kuchukua utambulisho wetu wa Kikristo kwa kutenda pamoja na Kristo ambaye anatungojea ili kututuza kulingana na chaguzi ambazo tumefanya katika dunia hii. Sisi sote tunaalikwa kwa maisha mapya ambayo Mungu anatupatia kwa neema yake, lakini bila kutenda kulingana na mapenzi yake, maisha mapya hayawezekani.

        Katika injili Yesu anaongea kwa watu kwa kutumia mifano ili kutueleza kuhusu nguvu ya Ufalme wa Mungu. Mfano wa kwanza ni kuhusu mbegu ambao unaota na kukua kwa nguvu yake mwenyewe; ushiriki wa binadamu ni kuupanda tu na kusubiri wakati wa mavuno ili kukusanya matunda. Wa pili ni kuhusu udogo wa kipimo cha mbegu ya haradali na ukuu wa matokeo yake. Kwa nini Yesu aliongelea watu akiitumia mifano? Chaguo la Yesu kwa njia hii ya kuongea ni kwa sababu yeye alijitambulisha na hali ya watu wanyenyekevu na tena akitumia vipengele vya hali hii ilikuwa ni halisi ili watu wafahamu ujumbe wake. Hivyo, kwa njia ya Yesu ya kuongea, mafumbo makubwa ya Ufalme wa Mungu yalipatikana kwa watu walio wadogo na wanyenyekevu.

     Katika ujumbe wake, Yesu hakujitangaza mwenyewe; yeye aliutangaza Ufalme wa Mungu. Ufalme ni kiini ya ujumbe wake. Kulingana na Yesu, hali na nguvu ya Ufalme wa Mungu haitegemei juhudi za binadamu, bali hiki ni tendo la neema ya Mungu inayotolewa kwa hiari. Kila mtu anaalikwa kutoa uwezo wake ili kusaidia kuujenga kwa Ufalme wa Mungu duniani, lakini ufalme huu ni kwanza tendo la Mungu nao unamtegemea yeye sio binadamu. Kwa upande wetu ni vizuri kutenda kama Mt. Yohana Calabria aliyechukua kama ahadi kutafuta kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake kupitia imani na kujisalimisha kabisa kwa riziki ya Mungu Baba. Mfano wake unatusaidia kufahamu kwamba hakuna kipaumbele kingine katika maisha yetu ili tuweze kupata furaha kamili.

      Watu wengi miongoni mwetu ni wakulima na mifano hii pamoja na kuwa mafundisho kuhusu hali ya Ufalme wa Mungu, tena ndiyo msaada ili waendelee kwa shughuli zao za kila siku kwa uvumilivu na imani katika tendo la Mungu. Mifano hii inatualika kuangalia mwendo wa ongezeko la mashamba katika uwanja, hasa kuhusu mahindi na maharagwe. Sisi sote tunajua kwamba baada ya kazi ya kwanza ya kupanda tunaitegemea mvua na nguvu ndani ya mbegu. Hiki ni kitendo cha Mungu anayethamini juhudi ya binadamu kama ushiriki katika uumbaji na kutubariki kwa mavuno mengi. Tumshukuru Mungu kwa nguvu ambayo anatupa ili kufanya kazi kwa uaminifu naye aendelee kutupatia Baraka zake kwa manufaa ya familia zetu.

Fr Ndega



sábado, 2 de junho de 2018

KUWA ‘EKARISTI’ ILI KULISHA ULIMWENGU



Kutafakari kuhusu Kutoka 24: 3-8; Ebr 9: 11-15; Mk 14: 12-16, 22-26


         Siku ya leo tunaalikwa kuadhimisha sikukuu ya Mwili na Damu ya Kristo, lililo fumbo la imani yetu. Hii ni nafasi maalum kuonyesha shukrani yetu na upendo wetu kwa zawadi kuu ya Ekaristi takatifu. Hii ni siku ya kutafakari kuhusu uwepo wa kweli wa Kristo katika ishara za mkate na divai. Ekaristi takatifu ni fumbo la kujisalimisha kwake kwa upendo kwa wokovu wa ulimwengu. Ekaristi ni adhimisho la fumbo la Mungu ambaye anawatumikia watu wake, yupo karibu nasi na ndani yetu. Hilo ni fumbo la ushirika ambao tunahusishwa kama washirika katika uhai wake. Ekaristi ni sakramenti ya Agano jipya na milele kupitia hilo Kristo anatuunganisha naye na miongoni mwetu wenyewe kama wana wa watu wapya wa Mungu lililo Kanisa.

      Masomo ya leo yanaongea kuhusu hali hii. Kulingana na somo la kwanza, agano ambalo Mungu alianzisha na watu wake lina kama msingi Neno lake ambalo watu alikubali kama mwongozo ili waweze kuishi kulingana na matarajio yake Mungu. Katika mwendo huu ni muhimu uwepo wa Musa kama mpatanishi mwema ili maneno ya Mungu yatangazwe kwa watu kikamilifu. Damu ya wanyama waliotoa kwa Mungu ikanyunyizwa juu ya watu ikithibitisha ahadi kati ya Mungu na watu wake. Somo la pili linaongea kwamba Kristo ndiye mpatanishi wa kipekee wa agano jipya na milele. Ukuhani wake ni mkubwa kuliko ukuhani wa agano la kale  kwa sababu una asili ya Mungu. Yeye hakuhitaji kumtolea Mungu damu ya sadaka ambayo inatoka kwa wanyama, bali alijitoa kama sadaka kamili na kupitia damu yake wanadamu wote walipata wokovu.

          Injili inasimulia tukio la Karamu ambayo Yesu akitumia ibada ya Wayahudi, alianzisha Ekaristi takatifu. Fumbo la usiku ule lilifunua hamu ya kiini ya moyo wa Yesu. Kweli Yeye alitaka kusherehekea pasaka na wanafunzi wake kwa sababu alikuwa na jambo muhimu la mwisho la kudhihirisha kwao. Aliwapa mafundisho yake ya mwisho akiwaalika kubaki kuungana naye kwa ajili ya mafanikio ya kazi yao: “Bila mimi hamwezi kufanya chochote”. Basi, kwa kutarajia, akihisi mwenye uhuru kabisa kwa kujitolea mwenyewe kwa ajili ya wale ambao aliwapenda mpaka upeo, "alitwaa mkate na kikombe, akashukuru, akawapa, akasema: twaeni huu ndio mwili wangu na hii ndiyo damu yangu. Vitendo hivi vya Yesu na wanafunzi wake vilivyofanyika katika hali ya kifamilia na amini ya kubadilishana kama mwaliko wa kuchukua ahadi pamoja.

          Mkataba kati ya Mungu na watu wake katika agano la Sinai ulikuta maana yake kamili na Yesu ambaye alifanya mkataba mpya, akianzisha Agano jipya kati ya Mungu na Watu wake wapya. Akitumia Ibada ya Wayahudi, Yesu alianzisha Ibada mpya, yaani Mlo wa Ekaristi, akitangaza kwa Wafuasi wake ukombozi kamili ambao ulikuwa ukija na kwamba alitamani kwa shauku kushiriki na marafiki zake. Katika karamu hii ya mwisho, Yesu alijitoa kama chakula na kinywaji, akionyesha maana ya kujisalimisha kwake kwa hiari msalabani. Kujisalimisha kwake kwa upendo na hiari kunakuwa tabia kamili na sharti kwa yeyote anayetaka kumfuata. Wanafunzi wake wakati watakaposherehekea Kuumega Mkate wataendelea mwendo huu kama ushiriki katika kujisalimisha kwa mwalimu Yesu wakipokea nguvu ili kujitolea wenyewe kama yeye alivyo.

     Huu ndio msingi wa misa takatifu yote. Hili ni maana ya imani yetu. Tunaalikwa kuadhimisha fumbo la Mwili na Damu ya Kristo kwa upendo na ahadi sawa Kristo alikuwa nayo aliposherehekea pamoja na wanafunzi wake. Yeye alianzisha Ekaristi akiutoa mwili na damu yake katika ibada, akiandaa wanafunzi wake kwa kujisalimisha kwake msalabani. Katika sakramenti hii Kanisa linaukuta utambulisho wake wa kweli kwa sababu linafanya upya ahadi yake na Yule aliye kichwa chake. Katika kila Ekaristi takatifu Kanisa linahisi moja na Kristo ili kuleta uzima wake duniani kote. Hii ndiyo Sakramenti inayolifanya Kanisa; hii ndiyo msingi na lengo la kazi yake.
    Katika Ekaristi uwepo wa Yesu ni hai na ufanisi. Yeye mwenyewe katika kila maadhimisho ya Ekaristi anatufanya kuona mabadiliko ambayo tunahitaji ili kuwa mashahidi wenye furaha wa ufufuko wake. Tunapoadhimisha Ekaristi tunabadilishwa kuwa kama Yule ambaye tunamsherekea kwa kukubali ukweli wa Fumbo hili kama “Pasaka ya Kristo katika pasaka yetu na pasaka yetu katika Pasaka ya Kristo”. Hivyo, baada ya kila adhimisho ya Ekaristi tuna changamoto ya kurudia shughuli za kila siku kama mashahidi wa Kristo anayetoa maisha yake kwa upendo ili wote wawe na maisha kamili. Basi, tumshukuru Mungu kwa uzoefu wa udugu tunaoishi katika kila misa takatifu tunayoadhimisha. Neema yake itusaidie kuishi uhusiano wa ndani na Yesu ili maisha yetu yawe kama vile yake, ‘ekaristi’ ili kulisha ulimwengu.

Fr Ndega

sábado, 26 de maio de 2018

KUWA MWANAFUNZI WA YESU KUNAMAANISHA KUWA MAKAO YA UTATU MTAKATIFU



Kum 4, 32-34.39-40; War 8, 14-17; Mt 28, 16-20


       Tunaalikwa kutafakari kuhusu fumbo la Utatu Mtakatifu. Utatu Mtakatifu ni fumbo la Mungu aliye ushirika wa Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Yeye yu ushirika wa upendo kwa maana Mungu ni upendo. Upendo ni tabia ya Mungu. Hivyo, “Mungu ni Utatu kwa sababu ndiye upendo” (L. C. Susin). Mungu yu wa kipekee lakini haishi peke yake kwa sababu alitaka kuwa na kuishi kwa ushirika. Uumbaji wote ni uenezi wa nafsi na wa fumbo lake. Viumbe vyote vinaitwa kuingia katika mwendo huu wa upendo na kuwa maonyesho ya wema wake. Tumsifu Mungu kwa ushirika wake wa upendo, atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu... 

       Tunapofanya ishara ya msalaba, yaani, “Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu”, tunaonyesha hisia yetu ya kuwa miliki ya Mungu na tena tunaongea kuhusu ukweli wa Mungu, ambaye yupo hapa na katika kila mahali. Yeye yu upendo aliye juu ya vyote na ndani ya vyote. Hivyo, anapatikana kwa wote lakini yeye ni fumbo daima kwa sababu hakuna lolote ambalo liweze kuweka mipaka kwako. Kulingana na Mtakatifu Agustino, “Mungu ni wa milele mno hata wakati yeye anapopatikana kuna yote ya kupatikana bado.” Kuna hadithi fulani ya Mtakatifu huyo ambayo inatusaidia kutafakari fumbo la Utatu Mtakatifu kama fumbo si la kufahamiwa bali la kukaribishwa. Ikiwa tunajifungua zaidi kwa fumbo hili tunaweza kuhisi zaidi tendo lake ndani yetu.

    “Siku moja Mtakatifu Agustino, aliye mchungaji na mwalimu wa kanisa, alikuwa akitembea katika pwani ya bahari, akijiuliza swali kuhusu fumbo la Utatu Mtakatifu, akisema, “inawezekanaje Mungu kuwako kama Mmoja na Utatu wakati huo huo?” Ghafla, alimwona mtoto mdogo aliyefanya shimo katika mchanga na kukimbia kwenye bahari, akachukua maji kidogo na kuyaweka shimoni. Baada ya kuangalia mchezo huu wa mtoto mdogo kwa mara nyingi, Agustino aliamua kumwuliza maana ya mchezo huo. Mtoto mdogo akamjibu akisema: “Najaribu kuweka maji yale yote ndani ya shimo hii”. Ameshangaa sana, Agustino akasema: “Hutapata kufanya hivyo kamwe!” Kisha, mtoto mdogo akamwambia akisema: “ni rahisi kwangu kuyaweka maji yale yote shimoni kuliko wewe upate kufahamu fumbo la Utatu Mtakatifu kwa akili yako. Mwishowe, mtoto mdogo alitoweka na Mtakatifu Agustino akajiambia: “Labda mtoto huyo angeweza kuwa ni malaika!”

         Ujumbe wa masomo ya siku ya leo unatusaidia kujifungua kwa fumbo hili. Kwa mfano, somo la kwanza linaongelea Mungu aliye karibu, ambaye anajifunua katika hali yetu ya kawaida kwa ishara ndizo halisi sana. Kuwa naye uhusiano wa mwana na imani ndiyo njia kamili ya kupata furaha na maisha mengi. Somo la pili linachukua tena hali ambayo tulitafakari wiki iliyopita, yaani tumepokea Roho ambaye anatufanya kuwa wana. Tendo la Roho ndani yetu anathibitisha kwamba sisi tu wana wa Mungu, na Yesu “hana aibu ya kuwafikiria kama ndugu wale ambao aliwatakasa”. Utakaso huu unamaanisha kuhusishwa katika ushirika mmoja ambao yeye anaishi pamoja na Baba, ushirika wa Mungu ambaye hajui kufanya jambo lingine isipokuwa kupenda.   

       Wanafunzi waliitwa na Yesu kuenda pamoja kwenye mahali fulani huko Galilaya. Kutoka mahali  huko walitumwa pamoja tena kuinjilisha kwa sababu ushahidi wa kwanza wa jumuiya ya wanafunzi wa Yesu ni umoja utakaohakikishwa na Roho yake. Kila mtu anaitwa kuweka juhudi kwa ajili ya kuusaidia umoja huu kama maana ya utambulisho. Tumezipokea zawadi kutoka kwa Mungu ili tuwe zawadi sisi kwa sisi na kuendeleza kuujenga mwili mmoja, ambao ni takatifu na hai kwa sababu ni Roho mmoja anayetenda ndani yake. Hivyo, uwepo wa Yesu ni muhimu sana kwa ajili ya nguvu na ufanisi wa wanafunzi wake, kwa maana mwili bila kichwa unakufa. Siku moja alisema, “Bila mimi hamuwezi kufanya chochote”.

      Ndiye Yesu peke yake na mamlaka aliyopokea kutoka kwa Baba ya kudhihirisha mpango wake wa wokovu. Alishiriki mamlaka haya na wanafunzi wake kwa ajili ya kufanya wanafunzi wapya miongoni mwa watu. Wanafunzi  walitumwa kama wajumbe wa habari njema kwa wanadamu wote kwa sababu injili haina mipaka. Yesu aliwaahidi kuandamana nao mpaka upeo. Ingawa uwepo wake wa mwili hauonekani tena, Roho wake anahakikisha ukaribu wake katika safari yao kwa sababu kama Yesu alitenda pamoja na Baba na Roho Mtakatifu, vivyo hivyo Roho huyo anatenda pamoja na Yesu na Baba. Ikiwa wanafunzi wanaruhusu kuongozwa na Roho huyo wanaweza kuwashirikisha wengi katika mpango wa Yesu ulio mpango wa Utatu Mtakatifu. Kuwa mwanafunzi wa Yesu ni kuwa makao ya Utatu Mtakatifu.

       Ujumbe wa uhusiano wa Utatu Mtakatifu ni msaada mkubwa ambao Ukristu unatoa kwa jamii yetu ambayo inaongozwa kwa njia ya ubinafsi na mashindano. Yesu alitukabidhi ujumbe wa upendo kama maana ya mambo yote. Tunaweza kuonyesha ukweli wa ujumbe huu ikiwa tunaishi kuungana naye (na  Utatu). Siku moja alisema “wote wawe na umoja; kama wewe Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu ili ulimwengu upate kusadiki.” Tunapoishi kwa uhusiano wa ndani na Yesu vivyo hivyo tunahisi ndani yetu tendo la Baba na Roho wake. Uzoefu wetu wa Yesu katika Ekaristi ni tena uzoefu wa Utatu Mtakatifu. Kulingana na fumbo hili, Mungu anatumikia, yeye yupo kati yetu na tena ndani yetu. Ndiye yeye mwenyewe anayetuunganisha naye na miongoni mwetu. Anafanya hivyo kwa sababu anataka tuwe washiriki katika uhai wake mwenyewe. Kwa hivyo, tuombe “Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mt...

Fr Ndega


ESSERE DISCEPOLO DI GESÙ È ESSERE DIMORA DELLA TRINITÀ



Riflessione a partire di Dt 4, 32-34.39-40; Rm 8, 14-17; Mt 28, 16-20


      Siamo invitati a riflettere sul mistero della Santissima Trinità. Trattasi della relazione di comunione del Dio che è Padre, Figlio e Spirito Santo. È una comunione d’amore perché Dio è amore. L’amore è l’identità di Dio. Così, “Dio è Trinità, perché è amore” (L. C. Susin). Dio è unico ma non vive da solo perché ha voluto vivere in comunione. Tutta la creazione scaturisce dal suo essere e dal suo mistero. Tutte le creature sono chiamate a entrare in questa dinamica d’amore che è la Trinità, ed essere manifestazione della sua bontà. Lodiamo Dio per la sua comunione d’amore, dicendo Gloria al Padre e del Figlio e dello Spirito Santo ...

      Quando facciamo il segno della croce, cioè, “Nel nome del Padre e del Figlio e dello Spirito Santo”, parliamo dell’identità di Dio ed esprimiamo il nostro senso di appartenenza a questo Dio che è presente in noi e in ogni luogo. Egli è amore che è sopra tutti e in tutti. Egli si rivela a tutti e si fa incontrare da tutti, ma continua ad essere un mistero perché non c'è nulla che possa imporre limiti al suo essere. Secondo S. Agostino, “Dio è tanto inesauribile che quando è trovato è ancora tutto da trovare”. Esiste un racconto su Sant’Agostino che ci aiuta a riflettere sulla Santissima Trinità come un mistero, non da essere capito ma accolto. Se ci consegniamo sempre più a questo mistero ancora di più possiamo sentire la sua azione in noi.

      “Un giorno Sant’Agostino – vescovo dottore della Chiesa - stava camminando sulla riva del mare, interrogandosi sul mistero della Santissima Trinità. Si domandava: “come Dio può essere uno e trino allo stesso tempo?” Improvvisamente, vide un bambino piccolo che faceva un buco nella sabbia e correva verso il mare, prendeva un po’ d’acqua e la metteva nel buco. Dopo aver osservato questo movimento del bambino per un po’ di tempo, Agostino decise di chiedere a lui il significato di questo gioco. Questi rispose dicendo: “Io cerco di mettere tutta quell’acqua in questo piccolo buco”. Molto stupito, Agostino disse: “Questo è impossibile!”. Allora il bambino gli disse: “E’ più facile per me mettere tutta quell’acqua in questo buco che tu possa capire il mistero della Santissima Trinità con la tua mente”. Alla fine, il bambino scomparve e S. Agostino disse a se stesso: ‘Questo bambino non era forse un angelo?!’”

     Il messaggio delle letture d’oggi ci conduce verso una apertura sempre maggiore a questo mistero. Per esempio, la prima lettura parla di un Dio vicino, che si rivela nel nostro quotidiano con dei segni molto concreti. Avere un rapporto filiale e, quindi, fiducioso con lui è la via giusta per la felicità, per la vita piena. La seconda lettura riprende la realtà che abbiamo riflettuto nella settimana scorsa, vale a dire: abbiamo ricevuto lo Spirito che ci rendi figli. L’azione dello Spirito in noi conferma la nostra filiazione divina, e Gesù “non si vergogna di chiamare fratelli coloro che ha santificato”. Questa santificazione vuol dire coinvolgimento nella stessa comunione che Lui vive con il Padre, comunione del Dio che non sa fare altra cosa eccetto amare.

      I discepoli sono stati chiamati da Gesù per andare insieme su un monte in Galilea. Da quel posto sono stati inviati per evangelizzare. Questo andare e fare le cose insieme è il primo segno che la comunità di discepoli di Gesù è chiamata a portare, animata dallo Spirito di unità. Ognuno è chiamato a mettere il proprio impegno per promuovere questa unità come ragione di identità. Noi abbiamo ricevuto doni da Dio perché siamo doni gli uni gli altri in vista dello sviluppo dell’unico corpo, che è vivo e santo perché è lo stesso Spirito che opera in esso. Così, l’unità a Gesù è fondamentale per la vita e l’efficacia dei suoi membri, perché il corpo senza il capo è morto. Un giorno egli disse ai suoi: “Senza di me non potete fare nulla”.

     Gesù solo ha autorità data dal Padre per rivelare il suo piano di salvezza. Egli ha condiviso questo potere con i suoi discepoli affinché loro possano fare nuovi discepoli tra la gente. I discepoli sono stati inviati come messaggeri di buona notizia a tutta l’umanità, perché il Vangelo non ha confini. Ma loro non andranno da soli. Gesù ha promesso di accompagnarli tutto il tempo. Anche se la sua presenza fisica non c’è più, il suo Spirito assicura la sua vicinanza nel loro cammino, perché se egli ha agito con il Padre e lo Spirito, nello stesso modo lo Spirito porterà con sé Gesù e il Padre. Se i discepoli si lasciano guidare dallo Spirito saranno capaci di coinvolgere molti altri nel progetto di Gesù che è il progetto Trinitario. Essere discepolo di Gesù è essere dimora della Trinità.

     Il messaggio sulla comunione trinitaria è la grande contribuzione che il cristianesimo offre per la nostra società che si lascia condurre dall’individualismo e dalla competizione. Gesù ci ha affidato il messaggio d’amore come ragione di tutte le cose. Noi siamo capaci di mostrare la verità di questo messaggio se rimaniamo uniti a lui (alla Trinità). Un giorno egli disse, pregando per i suoi: “Che loro siano una cosa sola; come tu, Padre, sei in me e io in te; siano anch’essi in noi, affinché il mondo creda”. Nell’intimità della nostra relazione con il Figlio, sentiamo anche in noi l’azione del Padre e dello Spirito. La nostra esperienza di Gesù nell’Eucaristia è un’esperienza della Santissima Trinità; Egli è tra noi e dentro di noi. Egli stesso ci unisce a se’ e ci unisce tra di noi. Lo fa perché vuole che siamo partecipi della sua stessa vita. Pertanto, preghiamo: Gloria al Padre e al Figlio e allo Spirito…

Fr Ndega