Mostrando postagens com marcador UJUMBE. Mostrar todas as postagens
Mostrando postagens com marcador UJUMBE. Mostrar todas as postagens

domingo, 19 de julho de 2015

MAFANIKIO YA UJUMBE

Amosi 7: 12-15; Waefeso 1: 3-14; Mk 6: 7-13

      Nabii Amosi alichaguliwa na Mungu ili kutabiri katika rali ralisi ya ugumu ya watu wa Israeli (Ufalme wa Kaskazini), ni kwamba, kukosekana kwa usawa katika jamii, udhalimu dhidi ya maskini na matumizi ya dini kulingana na mvuto binafsi ya mfalme. Badala ya hekalu la Yerusalemu (Ufalme Kusini) lilikuwa na hekalu nyingine likaloitwa Betheli kwa muda wa mfalme Yeroboamu wa II. Amosi alipoanza ujumbe wake katika mahali hapo, alikutana na kuhani wa hekalu la Betheli, aliyeitwa Amazia, ambaye alifanya upinzani dhidi ya unabii wa Amosi. Amazia ni aina ya mtu aliyelipwa ili kudumisha mfumu wa hekalu na kuhalalisha mfumu wa udhalimu wa mfalme. Kabla ya kutendewa vibaya, Amosi alidhihirisha maana na hamasa ya wito wake. Ujumbe wake wa nabii hautegemei ada, bali ni ari ya bure ya Mungu na ni mwaliko kwa bure.

       Somo la pili ni wimbo wa shukrani kwa Mungu ambaye ametubariki katika Kristu tangu mwanzo wa ulimwengu. Maana ya upendo wake, sisi ni wana na mabinti wake. Kwa ujumbe wa Yesu Kristu tumesamehewa dhambi zetu ili tustawi wito wetu kwa utakatifu. Wito huu ni sehemu ya mpango wa hekima na wema wa Mungu ambaye katika Kristu ametuchagua ili tuwe watu wake mwenyewe. Roho wa Mungu anatusaidia kuishi wito wetu kwa uaminifu na atatupatia utimizaji wa ahadi yake. Kulingana na Baraza ya Vatikano ya II utakatifu ni wito wa mambo yote. Sisi sote tunaitwa kwa wito huu. Kulingana na Mt Yohana Calabria, “hatuhitaji kufanya vitu vya ajabu ili kuwa takatifu. Tunaweza kufikia utakatifu kupitia hali ya kawaida maishani ya kila siku. Inatosha kwamba nia zetu kufanya chochote ziwe takatifu.”      
      Baada ya kumekataliwa kijijini chake, Yesu aliendelea ujumbe wake vijijini kandokando pale ambapo alikaribishwa sana. Aliweza kufanya kazi yake peke yake, bali hakutaka. Kwa hivyo aliwaita Mitume kumi na wawili kama washirika. Kabla ya kuwatuma kwa ujumbe, aliwapendekezea uzoefu wa ndani wa uzima; akawafundisha kwa uwezo aliopokea kutoka kwa Baba; akashirika nao unyeti wake kuhusu hali ya huzuni na mateso ya watu; kabla yao alitenda kwa mamlaka dhidi ya nguvu za maovu ambayo yaliwapooza watu, yakiwazuia kushiriki kikamilifu katika jamii. Hatimaye aliwapa maelekezo, hasa kuhusu mahitaji ya njia ya unyenyekevu wa maisha na akawatuma wawiliwawili.    

     Ari ya mwito inatoka kwa Yesu. Hakutafuta wenye nguvu au wenye adhiri katika jamii. Aliwachgua watu wanyenyekevu, wafanyakazi na walio makini sana kwa upya wa Mungu uliodhihirisha na Mwana wake. Yaliyomo ya maelekezo yaliyopewa na Yesu yanaufuata mwelekeo tofauti kabisa wa mawazo ya binadamu. Ili kuwa na mafanikio katika ujumbe, mitume walikuwa lazima kushinda baadhi ya tabia za binadamu ambazo zipo sana maishani mwetu: dhidi ya tabia ya kutenda ya mmoja mmoja, tunaalikwa kutenda pamoja na kusaidiana katika jumuiya na kwa wema wa jumuiya; dhidi ya tabia ya kutawala, Yesu anatupendekezea uwezo wake ili tutumikie watu; dhidi ya tabia ya kuwa na mali, Yesu anatupendekezea kujinyima, unyenyekevu na bure; dhidi ya tabia ya kulazimisha, tangazo letu ni pendekezo, pendekezo la toba, la ukombozi, la mabadiliko ya maisha. Kama Yesu sisi lazima kuheshimu uhuru wa wengine.   


     Ujumbe ulioshirikiwa na Yesu na wanafunzi wake ulichukuliwa kwa sisi sote ambao ni wafuasi wake wapya. Ni muhimu sana uwazi kwa msukumo wa Mungu ili tuwe na hamasa kuchukua njia ya unyenyekevu wa maisha yanayopendekezwa na Yesu, kwa ujasiri na hakika kama Amosi hata tutapokuta upinzani dhidi ya ari zetu. Matarajio ya Yesu ni kwamba pendekezo la toba ambalo tunawatangazia wengine liwe maonyesho ya mabadiliko ambayo tumehisi kupitia mkutano na huruma yake. Ili ukarimu na bure iwe tabia daima katika ujumbe wetu ili kupitia kwetu Mungu apatie maisha mengi kwa wote.    

Fr Ndega

domingo, 24 de maio de 2015

INGILI HAINA MPAKA


Mtdo 1, 1-11; Waef 4, 1-13; Marko 16, 15-20

       Sikukuu ya leo inatufafanulia fumbo la uwepo wa Yesu. Yesu hakuiacha mbingu alipokuja kwetu na hakutuacha alipochukuliwa mbinguni. Kupaa kwake Yesu kunaongea kuhusu njia mpya ya uwepo wake miongoni mwetu, kutangaza hatua mpya ya kazi yake. Huu ni wakati wa Kanisa, jumuiya ya wanafunzi wa Yesu. Ujumbe muhimu kuhusu huo ni wazi sana katika maandiko mawili ya Luka, Injili na Matendo ya Mitume. Katika Injili anazawadisha vitendo ya Yesu, na andiko la Matendo ya Mitume anazawadisha vitendo ya wanafunzi wake waliosaidiwa na Roho wake, aliye njia mpya ya uwepo wa Mungu miongoni mwao.    

        Mizimu ya Yesu kwa baadhi ya muda iliwahamasisha wanafunzi wake kujipatia maana ya uanafunzi, wakishinda hofu na mashaka kuhusu hali ya ufufuko wake. Uzoefu huo wote ulikuwa mpya sana kwao na Yesu alifahamu kwamba ilikuwa lazima kuwa na utulivu kwa sababu imani yao ndogo. Mwendo ulikuwa mrefu, lakini ufanisi sana, ukisababisha mabadiliko makubwa maishani mwa wanafunzi: kutokana na wanaume wenye hofu kwa mashahidi wenye ujasiri. Katika maneno ya mwisho kwao, Yesu aliwasaidia kufahamu uhusiano kati ya kila kitu alichotenda na kufundisha na hali halisi ya Ufalme wa Mungu. Hali halisi ya Ufalme wa Mungu ilidhihirishwa kupitia ishara za Yesu na inaendeleza kupitia matendo ya wale wanaouchukua ujumbe wako mpaka miisho ya ardhi. Kuongoja kujaa na nguvu kutoka kwa juu ni kujisalimisha kwa tendo la Mungu kama vyombo vya wokovu wake. Kazi hii haitoki kwa binadamu, bali inatoka kwa Mungu. Roho ilikuwapo katika mwanzo wa uumbaji, katika mwanzo wa ujumbe wa Yesu na lazima kuongoza kazi ya jamii ya wanafunzi wake.

          Ushahidi wa kwanza wa jamii ya wanafunzi ya Yesu ni umoja uliodhaminiwa na Roho ya Yesu. Kila mtu anaitwa kufanya bora ya mwenyewe ili kuhifadhi umoja huu kama maana ya utambulisho. Katika jamii tumezipokea zawadi kutoka kwa Mungu ili tuwe zawadi sisi kwa sisi, kujiunga nguvu ili kuchangia kwa kuendeleza kujenga kwa mwili mmoja, ambao ni takatifu na hai kwa sababu ni Roho moja inayotenda ndani yake. Kama hii fumbo la uwepo wa Yesu linadhihirishwa, kwa maana hatuwezi kutenganisha mwili kutoka kichwa.

          Yesu ni peke yake na mamlaka iliyopewa moja kwa moja kutoka kwa Baba ili kudhihirisha mpango wake wa wokovu. Alishiriki mamlaka hii na wanafunzi wake ili watumikie watu, wakidhamini maisha mengi kwa wote. Kigezo kupitia maisha mengi haya ni imani, ambayo huja kwetu kupitia hali ya ubatizo. Wanafunzi  walitumwa kama wajumbe wa habari njema kwa wanadamu wote kwa sababu injili haina mpaka. Yesu alikuwa amewaahidia kuandamana safary yao mpaka upeo. Ingawa uwepo wake wa mwili usionekana zaidi, Roho wake inadhaminiwa ili kuwahamasisha katika kazi yao. Uwepo wa Roho ya Yesu daima katika safari ya mitume yake na maishani ya wote waliomwamini umeyafanya maneno yao ufanisi kupitia ishara ningi na matendo mazuri.


         Malaika waliwaambia wanafunzi wa kwanza na wanatuambia siko ya leo: “mbona mmesimama mkitazama mbinguni?” hakika kama Wakristo tunahitaji kurudisha mtazamo wetu kwa Yesu, modeli yetu na kichwa chetu ili tuendeleze kazi yake kwa uaminifu, lakini hatuezi Kubaki komwa kutazama mbinguni. Hali halisi hii inaweza kumaanisha utazamaji na upooza. Bwana anatutaka wenye uangalifu na watendaji. “Wabarikiwa watumishi wale ambao watakuwa wakitumikia Bwana wao atakaporudi”. Maisha ya Kikristu ni tafakari na kitendo, imani na matendo. Ishara za uwepo utenzaji wa Yesu ni mapendo ya wale wanaomwamini na wanayofuata nyayo yake. Kitendo cha Roho Mtakatifu kifanye uzoefu wetu wa Yesu ufanisi katika maisha yetu ya kila siku, kuonyesha ishara za ahadi yetu naye na ujumbe wake.   

Fr. Ndega
Mapitio: Sara