Mostrando postagens com marcador SHERIA. Mostrar todas as postagens
Mostrando postagens com marcador SHERIA. Mostrar todas as postagens

sexta-feira, 2 de novembro de 2018

MPENDENI MUNGU NA JIRANI KAMA NILIVYOWAPENDA NINYI


Kutafakari kutoka Kum 6:2-6; Waeb 7:23-28; Marko 12,28-34


      Kulingana na Maandiko Matakatifu Mungu ana uhusiano maalum na Watu wa Israeli. Alianzisha agano na watu hawa, akiwapa baadhi ya mwongozo ili watembee salama na kuwa maisha mengi. Katika mazingira haya tunaweza kukiri kuzaliwa kwa Amri kumi. Kuishi Amri kulikuwa muhimu kwa Waisraeli ambao wanafikiria Neno la Mungu kuwa ni Sheria na Sheria kuwa ni Neno la Mungu. Wanaposema kwamba “Sheria ya Bwana ni kamili, faraja ya roho”, wanaongea kuhusu Neno la Mungu. Kuna uhusiano wa ndani kati ya Sheria na Neno, kwa sababu Amri za Sheria zinaonyesha utunzaji wa upendo wa Mungu ambaye anapoongea anaongoza njia kamili ya ukombozi na uzima. Kutii kwa Amri ni chanzo cha baraka maana huongoza kwa uzima, wakati kutotii kwa Amri kunaongoza kwa mauti.

      Basi, chanzo cha Amri ndio upendo wa Mungu. Yeye ni upendo na kupenda kwa hiari. Anafikia wote kwa uhusiano huu. Yeye anatarajia tuweze kumpenda pia kwa sababu aliweka moyoni mwa kila mtu uwezo huu tangu mwanzo mwa uumbaji. Upendo ni sheria yake ya kipekee. Sheria hii hailazimishi bali ndiyo zawadi na kuonyesha njia ya uhuru wa kweli. Hii ndiyo maana ya hotuba ya Musa kwa Watu wa Israeli katika somo la kwanza. Kupitia Musa, Mungu anaongea na Watu kutoka moyo kwa moyo, sababu Mungu anataka kuandika sheria yake mioyoni mwa wote. Yeyote anaishi sheria ya Mungu kwa kweli ikiwa anaweza kupenda. Kumpenda Mungu kunamaanisha kuishi kulingana na mapenzi yake. Katika somo la pili Kristo ni kuhani mkubwa kuliko makuhani wa Agano la Kale kwa maana alijitoa nafsi yake kwa upendo kwa ajili ya wenye dhambi wote, akitufundisha njia halisi ya kumpenda Mungu kwa kweli.

     Kando ya sheria kuu Wayahudi waliweka sheria nyingi ambazo polepole zilibadilisha makini kutoka muhimu sana. Jibu la Yesu ni kugundua tena jambo hili yaani, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote... Mpende jirani yako kama nafsi yako”. Kumpenda Mungu ni kwanza wa Amri zote, lakini Yesu aliiunganisha na upendo kwa jirani, akionyesha kwamba haiwezekani kumpenda Mungu kwa kweli bila kumpenda jirani. Kutokana na Amri ya kumpenda Mungu inaububujika upendo kwa jirani kama matokeo. Chanzo ni Mungu daima, kwa sababu alitupenda kwanza na kwa hiari. Ndio kutokana na njia ya Mungu ya kutupenda kwamba tunapaswa kuwapenda wengine. Hii ni changamoto kwa tamaduni yote hasa mahali ambapo uaminifu kwa familia na desturi kwa kawaida umekuwa kama amri ya kwanza.


     Hivyo, baadaye Yesu alitaka kufanya rahisi zaidi akijionyesha kama mfano. Kwa hivyo alibadilisha Amri mbili hizi ziwe moja peke yake, yaani tupendane kama yeye alivyotupenda. Kama Mungu alivyotupenda katika Kristo tunaalikwa kupendana kutoka kwa Kristo. Mtu ambaye anapenda kulingana na njia hii alifahamu umuhimu wa sheria naye sio mbali na Ufalme wa Mungu. Kwa kweli, mtu ambaye anamfuata Yesu hafuati sheria au mafundisho bali anamfuata Mtu aliyetupenda mpaka upeo. Tunajua kwamba katika jamii kuna sheria nyingi. Watu wenye hekima na upevu wanatii sheria lakini hawakuwa watumwa kwa sababu wanafahamu kwamba muhimu siyo sheria yenyewe bali ndiyo roho inayosukuma sheria na tabia mtu anayochukua mbele ya sheria. Lengo la sheria yote ni kuwafanya watu waishi vizuri, yaani kwa maelewano. Sheria inakuwa bila maana ikiwa lengo lake ni kuonea ama kusaidia marupurupu kwa baadhi ya watu kwa kubagua wengine. Hali hii ni pendekezo sio kwa jamii tu, bali pia kwa Kanisa, kwa jumuiya na kwa familia zetu. Changamoto kwetu leo ni kuweka juhudi ili sheria yote iwe chombo cha ndugu kama maonyesho ya upendo kwa Mungu na kwa jirani.    

Fr Ndega

terça-feira, 3 de março de 2015

MUHIMU ZAIDI YA SHERIA NI KUPENDANA


Utu uili muhimu wa biblia unatusaidia kuelewa vizuri ujumbe wa Kristo kama kuhani wa agano jipya na milele, kama vile Melkizedeki na Ibrahimu. Kuhusu Melkizedeki, alikuwa mfalme na kuhani, mfalme wa haki na amani. Hakuna mtu anaijua asili yake, lakini wote hukubali ukuhani wake. Kwa uhakika zaidi tunaalikwa kukubali ukuhani wa Kristo ambao una asili ya Mungu. Ukuhani wa Kristo ni rejeo kwa huduma yetu, kwa sababu kwa njia ya ubatizo wetu tulifungwa kwake kama sehemu za Mwili wake na tunaitwa kushiriki katika ukuhani wa pamoja ili kuwatumikia Watu wa Mungu.

Ibrahimu, katika uzoefu wake wa kujisalimisha anatumotisha kushukuru Mungu. Tabia ya kujisalimisha ni kurudisha kwa Bwana ambayo ni miliki yake. Kulingana na andiko hili, kuhani mkuu Melkizedeki anakutana na Ibrahimu na anambariki. Hivyo, baraka inatokea kabla ya sadaka ya Ibrahimu. Kama hii ni hatua ya neema ya Mungu katika maisha yetu; hutokea hata bila ufahamu kutoka kwetu na kabla ishara yoyote ya binadamu. Kama tunamtolea kitu hakiongezi chochote kwa Mungu, lakini kinaonyesha kutambua kwetu na shukrani yetu kabla ya zawadi nyingi ambazo tumepokea. Sadaka na kujisalimisha ni sehemu ya maisha yetu na maisha yetu ni kuwepo kwa sadaka ambayo tunatoa kwa Bwana. Sadaka yote hupata maana yake ya kweli katika sadaka ya Kristo, ambaye anajitoa kwa Mungu kwa wokovu wa wote.

Yesu ni Kuhani Mkuu ambaye anahisi huruma kabla ya hali halisi ya mateso ya watu. Yeye anahisi pia hasira kwa sababu ya kutojali na ukosefu wa haki kuhusu hali halisi hiyo. Yeye anapinga sheria ambayo iliishiwa kwa njia rasmi, kuzuia kuona mahitaji karibu. Kwake muhimu zaidi si sheria yenyewe, lakini roho ambayo ilimotisha sheria na tabia iliyochukuliwa kabla yake. Sheria inapoteza maana yake ya kweli wakati inatumika tu kuonea, kukuza maslahi ya binafsi. Kwa Yesu, sheria ya kweli inaikuza maisha na inawaongoza watu kufanya mambo mema kwa wengine. Wakati mwingine yeye anasema kwamba muhimu zaidi ya sheria ni kupendana. Yeyote amfuataye Yesu hafuati sheria au mafundisho, lakini anamfuata Mtu Yesu. Mtu Huyo hutufundisha kutumia kila sheria kama chombo cha udugu, ambacho upendo kwa Mungu na upendo kwa jirani unashuhudiwa kwa nguvu.

Fr. Ndega

Mapitio: Rose Mong’are