Mostrando postagens com marcador MAPENZI. Mostrar todas as postagens
Mostrando postagens com marcador MAPENZI. Mostrar todas as postagens

domingo, 21 de agosto de 2016

KUFANYA MAPENZI YA MUNGU NA KUPATA UZIMA


Kutafakari kuhusu Lk 13, 22-30

    Wakati wa safari ya kwenda Yerusalemu, Yesu alitumia nafasi ya kuwafundisha wanafunzi wake hasa kuhusu masharti ya kuingia katika ufalme wa mbinguni. Kwanza kabisa haitoshi kuwa wanafunzi wake ili kupata wokovu. Hivyo, aliwapendekezea mlango mwembamba kama changamoto. Ikiwa Yesu anajulisha mlango mwembamba ni kwa sababu pia kuna mlango mpana. Wakati Mt. Yohane Paulo wa II alipoongea na vijana katika mwaka wa 1993, alitofautisha vizuri njia hizi mbili, akisema: “kataeni barabara rahisi: barabara ya anasa, uhalifu, kudharau mazuri, na kukwepa wajibu. Ulevi na matumizi ya madawa ya kulevya na uasherati visiwe na nafasi katika maisha yenu. Pitieni mlango mwembamba. Chagua barabara ielekeayo kwenye uzima wa milele na furaha pamoja na Mungu.” Katika kifungu kingine Yesu alisema kwamba mlango mwembamba ni njia ambayo inaongoza kwenye uzima na wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo. “Huu ni mlango wa uvumilivu, busara, kujitoa, ukarimu, wema, shukrani na kazi”. Kuhusu mlango mpana, hii ni njia rahisi inayoongoza kwenye maangamizi na waendao njia hiyo ni wengi. Basi, ili wanafunzi wa Yesu waweze kupata mafanikio katika safari yao wapaswa kupitia mlango mwembamba.   

    Katika mazingira yetu mlango mwembamba ni ishara ya juhudi yetu ya kushinda mwelekeo mbaya wa maisha yetu na kuwatendea watu mema. Katika mwendo huu ndio sisi wa kwanza wa kupata mafanikio ama bahati mbaya, kwa sababu lile tunalofanya kwa ajili ya wengine linasababisha hali nzuri ama mbaya kwetu pia. Hadithi fulani inatusaidia kuelewa vizuri hali hii. “Siku moja mwandishi wa habari alimhoji mwenye shamba ambaye ameshinda mara ya tano mashindano kuhusu mahindi mazuri zaidi katika eneo hilo. Mwandishi alimwuliza swali akisema, “unapataje kuzaa mahindi bora kuliko wengine?” Mwenye shamba alijibu, mwendo huu ni rahisi sana; nina mazoea ya kushiriki mbegu zangu nzuri na majirani wangu.” Mwandishi aliendelea kwa swali akisema, “Kwa nini unashiriki mbegu zako nzuri na majirani wako ikiwa hao wanashindana pia katika mashindano haya pamoja?” “kwa sababu ni upepo ambao unasambaza poleni ya mahindi na tena ni upepo ambao unaweka poleni mashambani na unafanya mbegu zikue. Ikiwa majirani wangu watakuwa na mahindi mabaya, upepo utasambaza poleni mbaya shambani kwangu nayo mahindi yangu yatakua mbaya. Basi ili mahindi yangu yawe mazuri ninapaswa kuwasaidia majirani wangu wote ili wawe na mbegu nzuri.”

      Basi, lile zuri ambalo tunatarajia kwa maisha yetu tunapaswa kusaidia kwa ajili ya wengine. Katika mwendo huu hatuwezi kuitafuta furaha kwa njia ya ubinafsi. Ikiwa tunataka kuwa wenye furaha, tunapaswa kuisaidia hali hii nzuri kwa wale wanaoishi karibu nasi nao wako na shida sawa nasi. Tunapaswa kushinda mwelekeo wa jamii wa kufikiria wengine kama washindani nasi. Wengine sio washindani, bali ndugu. Kujaribu kupata upendeleo tukiwavuruga wengine ni udhalimu na kutuacha mbali sana na matarajio ya Yesu. Ikiwa tuko mbali na matarajio ya Yesu, matokeo yatakuwa mbali sana na yale tuliyotarajia kwa maisha yetu. Tunaweza kuongea vizuri sana kuhusu Yesu ili kuonyesha kwamba tunamjua Yeye na Biblia pia. Tunaweza hata kufikiri kwamba kuongea bora kuliko wengine kunawezekana kuwa faida ili tupokee baadhi ya tuzo kutoka kwa Mungu. Lakini, kulingana na andiko hili, maneno hayatoshi kuingia katika ufalme wa Mungu. Wokovu si astahili yetu, lakini hii ni zawadi ya ukarimu wa Mungu.


         Je, inawezekanaje tuseme kwamba tunamjua Yesu naye aseme kwamba hatujui sisi?” Hii ni kwa sababu katika biblia kitenzi kujua kinamaanisha uhusiano wa ndani, uzoefu wa kina ambao ni muhimu sana katika safari yetu ya wanafunzi wa Yesu. Ikiwa anasema kwamba hatujui sisi ni kwa sababu sisi hatumjui yeye. Katika mwendo huu hakuna ahadi/makubaliano kuhusu pendekezo lake, hakuna utambulisho. Hatuwezi kuwa wanafunzi wa Yeu kupitia maneno peke yake. Ushuhuda wa maisha unathamini zaidi kuliko maneno. Tukijifikiria bora kuliko wengine haituhakikishia wokovu. Kila kitu tunachofanya kinasababisha matokeo makubwa kwetu na katika hali iliyo kandokando yetu. Kwa maneno mengine, kufikia mafanikio ama bahati mbaya kwa maisha yetu kunatutegemea sisi wenyewe; huu ni uamuzi wetu. Neema ya Mungu ituongoze ili tuweze kufanya mapenzi yake na kupata uhai. 

Fr Ndega
Mapitio na marekebisho: Serah

sexta-feira, 27 de março de 2015

NIKO HAPA ILI KUFANYA MAPENZI YAKO

Kutafakari kutoka Mk 11: 1-10; Isa 50: 4-7; Flp 2: 6-11; Mk14: 1-15: 47

Yesu, anayechukua kuwa Masihi mnyenyekevu na maskini, anatangazwa kama mfalme na mshindi katika kuingia kwake Yerusalemu. Anakubali ishara hii ya umati wa watu hata kujua kwamba ataachwa peke yake kwa kunywa kikombe cha mateso na huzuni ili kufanya mapenzi ya Mungu. Yeye ni mtumishi wa Bwana kwa ubora, ambaye hata anahisi kuachwa, alibaki mwaminifu kwa mpango wa Mungu, akiisalimisha maisha yake kwa imani jumla mikononi mwake.
Kulingana na somo la kwanza, mtumishi wa Bwana ni mwaminifu kwa kazi ambayo Bwana alimkabidhi. Mtumishi anaishi wito wake kwa shauku, kuchukua matokeo ya uamuzi wake. Yeye lazima kuvumilia matusi, mateso, mshangao na kukataliwa, lakini dhamana ya mafanikio katika kazi yake ni uwepo wa Bwana daima na mwaminifu. Katika kilimo ya utambulisho wake wa mtumishi, yeye ni wazi kabisa kwa mapenzi ya Mungu ambaye anamwongea kila siku ili, kwa njia ya uzoefu wa Neno hilo, aweze kutenda kama mwanafunzi. Ni hayo ambayo Mtakatifu Paulo anaomba kwa jumuiya ya Wafilipi, kuonyesha mfano wa Kristo aliyechagua kuwa mtumishi, akikubali fedheha na mateso ili kufanya mapenzi ya Mungu. Hii ilikuwa njia ya utukufu wa Mwana wa Mungu na pendekezo ya kiradikali kwa wale ambao wanataka kumfuata kwa uaminifu.
Andiko la mateso kulingana na Marko ni mwanzo simulizi na linaonyesha maelezo muhimu kwa safari yetu kama wafuasi wa Yesu. Tuanze kuhusu uwepo wa mwanamke katika mwanzo na mwisho wa andiko hili. Wakati wa maisha yake ya umma, Yesu aliruhusu uwepo wa wanawake daima na kikamilifu katika kazi yake. Kupitia ishara yake ya mwaliko na kuthamini ya uwepo wao katika kazi yake, alijipatia heshima yao na anawazawadisha kama rejea katika mwendo wa uinjilishaji. Katika mwanzo wa andiko hili, tunaalikwa kutafakari kuhusu ishara ya kushangaza ya upendo na heshima ya mwanamke kwa Yesu, akitumia marashi ghali, kubadilisha mawazo na hali nyumbani pale. Kwa ishara hii, anafundisha kwamba kumfuata Yesu ni kutumia bora ya mwenyewe kwa upendo. Katika mwisho wa simulizi hii wanawake hawana hofu ya matokeo ya utambulisho wao na Mwalimu. Ushahidi wao ni mwaliko kwa kuendeleza uamuzi wa kumfuata Yesu hadi mwisho.
Yesu alisalitiwa, akaachwa, akapigwa, akaaibishwa, akatukanwa na akabaki kimya. Kupitia ukimya huu anaonyesha nguvu yake. Anaamua kusema tu ili kuthibitisha utambulisho wake wa Masihi na uhusiano ndani na Mungu Baba yake. Kupitia uhusiano huu ndani, ulioonyeshwa kwa maombi yake katika Bustani Gethsemane, anajihamasisha kukubaliana na msalaba na kufanya mapenzi ya Mungu, kujisalimisha mikononi mwake kwa tabia ya imani na upendo jumla. Kifo chake hakikutakwa kwa Baba yake, lakini ishara yake ya upendo hadi matokeo ya mwisho ilikubaliwa na ikajibiwa kupitia ufufuo mtukufu kutoka kwa wafu.
Kabla ya ukatili ya wale ambao walimsulubisha, Yesu hakuitikia, akijidhihirisha mfano wa mtu asiyekuwa na fujo, akitangaza kwamba wafuasi wake hawangepigana kwa sababu ufalme wake si wa dunia hii. Kama hii analaumu kila aina ya ukatili. Kama chembe ya ngano ambayo inakufa ili kuzaa matunda mengi, Yesu alikubali kuteseka na kufa kwa utambulisho na mshikamano wake na wanaosumbuka na waliosulubiwa wa ulimwengu huu ili kuwapa maisha mapya. Hivyo, ishara yake inaendeleza kuhamasisha wanaume na wanawake kujikataa, kuichukua misalaba yao na kuzifuata nyayo zake, kuwa wapatikana kwa kila kitu kwa ajili ya Ufalme wa Mungu. Kwa maadhimisho haya ya Ekaristi tunaalikwa kuanza Wiki hii takatifu kuhamasishwa sana kumtambua na kumtangaza Yesu kama Mwokozi wetu, kumwandama katika uaminifu wake kwa mpango wa Mungu na kushinda majaribu ya usaliti na kanusho kuwepo katika safari yetu daima. Mfano wake wa unyenyekevu, utupu na kujisalimisha mikononi mwa Mungu kutuhamasishe kuisalimisha maisha kabisa kwa mema ya wengine.

Fr. Ndega
Mapitio: Rose Mong'are