Mostrando postagens com marcador UWEPO. Mostrar todas as postagens
Mostrando postagens com marcador UWEPO. Mostrar todas as postagens

sábado, 29 de abril de 2017

UWEPO HAI NA UFANISI WA KRISTO ULIMWENGUNI


Kutafakari kuhusu Mat 2, 14a.22-33; 1Pd 1, 17-21; Lk 24, 13-35



Yesu alishiriki uwezo wake na wanafunzi wake akiwawezesha waendelee kazi yake. Kwa msaada wa Roho Mtakatifu, hasa katika siku ya Pentekoste, walitangaza kwa furaha uzoefu walioishi pamoja na mwalimu wao na ushindi wake juu ya mauti kwa uwezo wa Mungu. Tangazo hili ni mwaliko wa tumaini kwa sababu ushindi wa Yesu unatoa nafasi ya wokovu kwa wote. Kwa sababu ya Kristo imani yetu na tumaini letu linamwelekea Mungu ndiye Baba na kutaka tutende kulingana na mfano wa Mwanawe. Ingawa Yesu haonekani tena kwa macho, yeye anaweza kutambuliwa kwa matendo yetu mema hasa tunaposikiliza neno na kusherehekea Ekaristi. 

Mazungumzo ambayo injili inatujulisha ni mamoja kati ya mazungumzo ya ajabu na ya kamili ya Biblia. Hapo tuko na mwendo wetu wa upevu wa imani na sehemu za sherehe ya Ekaristi takatifu, yaani hali ya jumuiya inayokusanyika kwa jina la Bwana, uwepo wa Bwana Mfufuka anayetueleza Maandiko Matakatifu na kuumega mkate kwa kutualika kuendelea kama yeye alivyo.  

Tuko na wanafunzi wake wawili walikuwa wakielekea mji uitwao Emau, Kilomita 11 kutoka Yerusalemu. Wanafunzi walihuzunika sana, wamekata tamaa, wamekufa moyo na wakaiacha jumuiya na kurudi nyumbani, wakiwa tayari kusahau kila kitu walichoshiriki pamoja na Yesu. Walitarajia Masihi mtukufu na mfalme mwenye nguvu, lakini matokeo yalikuwa mbali sana na matarajio yao: mtu mpendwa alishindwa na akafa msalabani. Hakukuwa chochote cha kufanya isipokuwa kurudi kwa maisha waliyoyajua kabla ya kukutana na Yesu.

Ghafla alitokea mtu mgeni, ambaye alitembea pamoja nao na kuongea nao kuhusu matokeo ya hivi punde, yaani Yesu aliye nabii mwenye nguvu katika kazi na maneno mbele ya Mungu na watu, lakini alikuwa na mwisho usiotarajiwa. Huyo Mtu Hija aliyatafsiri Maandiko ambayo yanazungumza kuhusu Masihi. Walimsikiliza kwa uangalifu na mioyo yao ilianza kuchoma. Hatimaye, wanafunzi walifika nyumbani na kumwalika: “Kaa pamoja nasi, Bwana”!

Baada ya kulikaribisha Neno la Mtu hija, walimkaribisha nyumbani kwao. Yule mgeni alikubali kuingia sio kwa kukaa pamoja nao usiku mmoja tu, bali kubaki nao daima. Wakati wao walikuwako mezani,  mtu Hija  alifanya ishara inayojulikana, ishara ya karamu ya mwisho, wakati Yesu alipoanzisha Ekaristi. Macho ya wanafunzi yalifunguliwa na kumtambua Bwana Mfufuka. Hivyo Neno linaichoma mioyo; kuumega mkate hufanya kufungua macho. Kristo alitoweka maana jumuiya imekwisha pata ishara halisi za uwepo wake, yaani Neno lake na Mkate Uliomegeka. Asiyeonekana kwa macho, Bwana ndiye kuwepo na kubaki daima. Sasa ni wakati wa kushuhudia.

Yesu yu hai na kuandamana na binadamu katika safari yetu, ingawa hatambuliwi daima. Anajifanya kujulikana katika uzoefu wa kuumega mkate. Kama wanafunzi wake tunahitaji kuwa pamoja naye, kujiruhusu kuandamana naye, kusikiliza maneno yake na kumwalika kukaa nasi. Ni thamani yake kukaa nasi na kutuonyesha njia ya kweli ya kuishi. “Ni maonyesho haya ambayo Wakristo wa kwanza walitumia kuonyesha ushirika wao wa Ekaristi. Kwa kufanya hivyo walimaanisha kwamba wote ambao wanakula mkate mmoja uliomegwa, yaani Kristo, wanaingia katika ushirika pamoja naye na kufanya mwili mmoja naye” (CCC 1329).


Katika safari yetu ya imani hatuko peke yetu kamwe. Yesu anatujia na kutembea pamoja nasi. Yeye anapatikana kwetu hasa wakati tunapokata tamaa na kutaka kuacha ahadi yetu kabisa. Yeye anatusikiliza na kutuongoza kwa neno lake ambalo linachoma mioyo yetu ili tuweze kumtambua katika Ekaristi na kuishi hali hii katika uzoefu wetu wa kila siku. Ndio uzoefu huu unaotufanya kuwa mashahidi wenye furaha na ujasiri wa uwepo wake hai na ufanisi kati yetu.   

Fr Ndega

quarta-feira, 22 de abril de 2015

UWEPO HAI

Kutafakari Kutoka Matendo ya Mitume 3:13-15, 17-19a 1Yohana 2:1-5a; Luka 24:35-48

        Ikiwa Yesu hakuwa amefufuka imani ya Kikristu ingekuwa utupu, haina maana. Lakini Yesu alifufuka na hiyo ni maana ya uanafunzi na ushahidi wa mitume. Tangazo la tukio hili kuu lilifanywa na Mitume kwa shauku na furaha kubwa, wakiazimu njia mpya ya kuishi. Wakati Petro alianzisha hotuba yake kwa Wayahudi, alimsifu Mungu, ambaye kwa nguvu yake, alimfufua mtumishi wake Yesu kutoka kwa wafu. Petro aliwakumbusha pia kwamba ingawa watu hao walimkataa Yesu, hawakukataliwa na Yesu, ambaye alitarajia mabadiliko yao, akiwatolea uwezekano wa ushiriki katika uhai wake wenyewe. Wayahudi walifanya chaguo mbaya kwa sababu ujinga wao kuhusu utambulisho wa Yesu. Lakini, kupitia huruma ya Mungu katika Yesu, wana pia nafasi mpya ya kuishi. Mtakatifu Yohana anathibitisha, katika waraka wake, kwamba kupitia upatanishi wa Yesu huruma hii ya Mungu inafikika kwa wote. Utii kwa Neno la Mungu na kuishi amri yake ya upendo ni vigezo kumjua na kuipitia huruma yake.
Mwanzo wa injili ya siku ya leo ni mwendelezo wa uzoefu uliishi na wanafunzi wa Emau. Walikuwa wakisimulia toleo lao la tukio kwa wengine kwa shauku na furaha wakati ghafla Yesu mwenyewe akaonekana katikati yao, akithibitisha simulizi lao na akiwatolea amani kwa wote. Uzoefu  wa kushiriki pamoja mkate sasa unaenezeka kwa kushiriki kwa maisha na udugu. Katika wakati wa kwanza, hofu na ziada ya shaka iliwazuia kumtambua. Kosa la uhusiano wa ndani kuhusu njia mpya ya uwepo wa Bwana lilisababisha upinzani mioyoni mwao, likiwafanya kumfikiria roho. Yesu alikemea tabia zao na aliwaonyesha ishara za ushindi wake, ni kwamba, mikono na miguu. Alitenda kwa uvumilivu, akiheshimu mwendo polepole wa ufahamu wao na akafungua akili yao kupitia tafsiri haki ya Maandiko Matakatifu kuhusu yeye mwenyewe kama masiya aliyeteseka na aliyetukuzwa. Yesu si pepo; yeye ni uwepo hai, ambaye anakula na wapendwa ili kujipatia utambulisho wao wa wanafunzi na kuwahamasisha kwa kazi. Sasa wana sababu zenye nguvu kwa kuchukua tena njia ya uanafunzi na kuwa mashahidi wa kweli ili kutangaza mahitaji ya kutubu na maridhiano na Mungu na miongoni mwa watu.       
Kupitia uzoefu wa wanafunzi hao tunatambua kwamba furaha ya mkutano na Yesu lazima kutangazwa na unahamasisha uzoefu wa jumuiya, kuijalisha kwa maana. Kwa hali hii uzoefu wa jumuiya na uzoefu wa ufufuko ni uhusiano kwa sababu Bwana Mfufuka yupo katikati ya jumuiya. Bila usaidizi wa jumuiya tuna ugumu kutambua uwepo wa Bwana Mfufuka. Jumuiya hutupa uungaji mkono kwa ushahidi wa kweli na wenye fahari daima kuhusu mkutano na Bwana, kuweza uzoefu uliojaa umaana kwa wale ambao lazima kuwa mashahidi wake. Ni yeye ambaye anawaelimisha ufahamu wetu ili tuweze kuelewa Maandiko Matakatifu, kukuta katika Haya maana ya kweli ya uwepo wake miongoni mwetu. Alikubali uzoefu wa msalaba kwa mshikamano na waliosulibiwa wa wakati wote. Basi, hakuna mtu anaweza kudai kumfuata Kristu bila msalaba. Hakuna mtu anaweza kudai kuwa mwanafunzi wa kweli bila kuchukua ajili ambayo Mwalimu Yesu alichukua. Ufufuko wa Yesu ulifanya upya matumaini yote na ulithibitisha kwamba mateso, maovu na mauti hayatakwi na Mungu, ambaye anaweza kubadilisha bahati mbaya kwa neema, kufanya kuangaza uhai ambapo mauti tu yalipo.

Mungu wa uhai anatuita kuishi katika jumuiya na yeye yupo katikati yetu ili kuwa rejea ya maisha yetu na kutufanya vyombo vya amani yake. Kama wanafunzi wa kwanza, sisi pia tunakabiliwa na hali halisi ambazo zinatuletea wasiwasi na mashaka. Wakati tuko tayari kwa uzoefu wa mkutano binafsi na Bwana Mfufuka, kupitia Ekaristi na kushiriki kwa udugu, tunaimarishwa katika imani na sisi huisaidia imani ya jumuiya. Uzoefu unatuweza kushinda vikwazo njiani, kutubadilisha kwa mashahidi ya upendo ambao huyazaa maisha. Adhimisho la Ekaristi hili lituhamasishe kwa uzoefu wa mkutano na Bwana Mfufuka yupo miongoni mwetu. Ikiwa Uzoefu una nguvu, ushahidi utakuwa ufanisi.  

Fr Ndega
Mapitio: Rose Mong'are