sábado, 20 de outubro de 2018

UKUU WA KWELI NI KUTUMIKIA KWA UNYENYEKEVU NA UKARIMU



Kutafakari kutoka Is 53, 10-11; Waeb 4, 14-16; Mk 10, 35-45

     Maisha ya yule ambaye anamtumikia Bwana yana maana kubwa. Yote ambayo anafanya yalenga kufunua mapenzi ya Yule ambaye alimwalika kuwa mtumishi wake. Kwa sababu ya kujisalimisha kwake kwa upendo watu wengi wataokolewa (andiko la kwanza). Huyo ndiye Kuhani mkuu ambaye tunahitaji, yaani mtu kama sisi, ambaye anachukua hali yetu ya udhaifu - ila dhambi – ili kutuonyesha njia kamili ya kushinda hali hii na majaribu yote yanayotuzuia kuonja neema ya Mungu na kuishi kulingana na mapenzi yake (andiko la pili).

         Katika injili, ndugu wawili, yaani Yakobo na Yohane walimwendea Yesu na kumwomba kitu. Walitaka kuketi mmoja mkono wake wa kuume na mwingine mkono wake wa kushoto katika utukufu wake. Ombi hili linadhihirisha kwamba wanafunzi wake walishindwa kufahamu utambulisho na utume wa Mwalimu wao. Ni muhimu kukumbuka kwamba hali hii ilitokea baada ya ufunuo wa Yesu kuhusu mambo yatakayomtokea yeye katika Yerusalemu, yaani mateso, kifo na kisha kufufuka. Katika kipindi kingine, wakati Yesu alipoongea kuhusu matukio muhimu hayo, wanafunzi walijadiliana kuhusu ni nani ndiye mkuu kati yao, wakionyesha kwamba mawazo na matarajio yao yalikuwapo bado mbali sana na pendekezo la Mwalimu Yesu. Hivyo, yeye alipaswa kuwa na uvumilivu sana mbele ya ugumu wa wale aliowachagua kama washirika. Hata hivyo, aliweka halisi daima masharti ya kumfuata. 

         Kwa wanafunzi wa Yesu, sehemu muhimu ya tangazo lake ndio utukufu kwa sababu walitafuta kuwa wahusika wakuu. Wengine kumi walikasirika kwa sababu walitafuta mambo sawa na wote wawili nao hawakukubali kubaki nyuma. Kwa maneno mengine, wote walikuwa wazi katika kutafuta kwao, yaani walitafuta msimamo, umaarufu na upendeleo, lakini walichagua Mtu sio kamili wa kumfuata ili kutimiza lengo hili kwa sababu mantiki ya Yesu ni tofauti. Mbele ya hali hii ya mgawanyiko kwa sababu ya ghasia ya rejeo la maisha, Yesu aliwaalika tena kama mara ya kwanza na kusahihisha matarajio yao potovu: “anaondosha fikra zao walizojijengea wenyewe.” Njia ya maisha yake ina mwelekeo tofauti na wa dunia. “Katika ufalme wa Yesu, wale walio viongozi hawapo ili kuwanyonya wengine au kutegemea heshima na utumishi kutoka kwa watu wao, bali viongozi ndiyo huwa watumishi wa watu.”

       Basi, mantiki ya Yesu ndiyo mantiki ya utumishi unaokuta katika maisha yake rejeo lake: “Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.” Hali hii ambayo ilishirikisha maisha yake wakati wote inakuwa ni rejeo kwa maisha ya wale ambao wanatamani kumfuata kwa uaminifu: “Yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote; na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.” Hakuna njia nyingine ili mtu aweze kupata maana kamili ya maisha. Yeyote anayeamua kumfuata Yesu hawezi kuendelea kufikiri na kutenda kama mtu wa zamani.

        “Yesu anakumbana na upinzani mkali huko Yerusalemu na kumfanya apoteze maisha yake. Lakini jambo hilo Yesu anaona ni huduma ya upendo kwa watu wake (Mk 10:45).” Ndiyo kupitia imani katika Kristo na msukumo kutoka Neno lake kwamba yeyote anaweza kukabiliana na taabu, kukataa na mateso bila kukata tamaa. Hivyo, kuishi au kulima wito wa mtumishi kwa uaminifu sio rahisi kwa sababu kuna vitu vingi dhidi ya uamuzi wetu, yaani mawazo kandokando yetu kwa kawaida ni tofauti na pendekezo la injili; upinzani kutoka kwa wengine hata familia; mwelekeo wa kibinadamu ambao ndani yetu unatuimarisha kutafuta kutumikiwa badala ya kutumikia; kutokuwa na imani yenye nguvu na kosa la uvumilivu katika matendo mazuri, n.k.

        Vitu hivi vyote ni sehemu ya safari yetu pamoja na hamu yetu ya kumfuata Yesu kwa uaminifu. Lakini hatusahau kwamba hatutembei peke yetu. Yule aliyekubali “kujitoa kama zawadi kwa watu wote” ndiye mfano wetu na kutuhakikishia msaada wake ili tudumu katika utumishi kwa ajili ya wengine hata mbele ya kutokuelewana na taabu. Ikiwa ndio upendo ambao unatoa maana ya maisha, hakuna njia nyingine ya kuishi kwa maana ila kupitia utumishi kwa unyenyekevu na kwa ukarimu kwa wengine ulio maonyesho halisi ya upendo na utambulisho na Yule ambaye “alikufa na kufufuka kwa ajili yetu, inatoa mwenyewe kwa uhuru wetu na kuuimarisha kutafuta, kugundua na kutangaza maana hii ya kweli na kamili.”

Fr Ndega


sábado, 6 de outubro de 2018

“BILA UAMINIFU HAKUNA FURAHA”



Kutafakari kuhusu Mw 2: 18-24 Mk 10: 2-16


         Mwanzoni mwa injili ya leo Yesu alikuwa akiwafundisha watu kama ilivyokuwa desturi yake. Ghafla baadhi ya Mafarisayo walimwendea wakimjaribu. Jambo lilikuwa kuhusu talaka. Yesu aliitambua nia yao mbaya, lakini aliwatendea mema, akiwasikiliza kwa utulivu na kuthamini juhudi zao za kumwuliza maswali. Katika mazungumzo na Yesu shida yao ya pekee ilikuwa mtazamo upungufu kuhusu ndoa na familia. Yesu alisahihisha mtazamo huo, akiwakumbusha mpango wa kiasili wa Mungu kwa mwanamume na mwanamke. Aliongea pia kuhusu uzinzi kama matokeo ya talaka na kuonyesha uhusiano maalum na watoto wadogo ambao wanastahili kuheshimiwa na kuthaminiwa ili waweze kukua kwa usalama na furaha.

      Baadhi ya Mafarisayo wanatumia sheria ya Musa kumjaribu Yesu. Kulingana na mawazo yao, Sheria hiyo inaruhusu talaka, lakini Yesu anayakataa hayo. Kwa nini Yesu ana msimamo tofauti kwa uhusiano na jambo hili la Sheria? Kulingana na Kitabu cha Kumbukumbu la Sheria, sura 24, mwanamume aliweza kumpatia mkewe talaka ikiwa hakupendezwa naye kwa sababu ameona kwake kitu kisichofaa. Mwanamke alikuwa na nafasi chache za kutoa talaka kwa mmewe, mfano mwanaume akiugua ukoma. Katika mazingira haya hali ya mwanamke ilikuwa ngumu sana kwa sababu daima alionewa na daima alitegemea huruma tu ya mwanamume. Lakini Yesu aliwasaidia kufikiri vizuri kwa sababu Sheria zimewekwa kwa manufaa ya watu na si watu kwa ajili ya sheria.

        Msimamo wa Yesu ni wazi sana. Yeye alikuja kudhihirisha mpango wa kiasili wa Mungu na kulingana na mpango huu, wote mme na mke wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu na Mungu ameweka upendo asili unaowafanya watamaniane na hatimaye kuwaacha wazazi wao, kuungana na kuwa mwili mmoja. Jambo hili linaonyesha kuwa mwanaume hana haki ya kuamua atakavyo kwa mkewe, mfano kumwacha mke wake kwa muda wowote anaotaka. Hivyo kuungana kwao kunamaanisha kuwa hawawezi kuachana au kutenganishwa. Lengo kuu la Yesu, ni kukarabati nafasi ya mwanamke ulioharibiwa na sheria. Kulingana na Yesu Mwanamke ana haki ya kuheshimiwa katika maisha ya ndoa na si kutendewa na kumilikiwa kama chombo tu. Nia ya Mungu ni kuwa mume na mke waendelee kukua katika upendo na kupata uzima wa milele. Nasi tunaweza kuushiriki pia mpango huu wa kuishi maisha ya umoja katika familia na jumuiya zetu.

      Thamani ya kibinadamu ya kupenda na kupendwa ni maana ya uzoefu wa ndoa na familia. Familia ni msingi wa uzoefu wa kibinadamu na yoyote ambayo ni dhidi ya kanuni hii ni marufuku katika biblia. Kwa hiyo “Usizini” ni moja miongoni mwa Amri Kumi. Kwa nini uzinzi hutishia familia? Uzinzi unaweza kuharibu familia kwa sababu unaweza kusababisha ujauzito na kuzaliwa kwa mtoto. Mtoto huyo ataanza safari ya maisha pasipo familia. Ikiwa uzinzi hauharibu familia, mara nyingi unasababisha madhara ya kutisha ndoa, kama hisia ya usaliti na upotevu wa itibari kwa kuonyesha kwamba uzinzi unamaanisha maisha ya ulaghai. Ni lazima kuwa macho kwa baadhi ya aina za urafiki. Wakati mume au mke ana urafiki fulani ambao unaanzisha uhusiano wa nguvu kuliko ule mtu anaoishi na mke au mume ni ngumu sana kuuepuka uzinzi. Wakati mume au mke ana ngono na mwingine kuliko mkewe/mumewe, mawazo kuhusu yule mtu ni daima na mawazo kuhusu jinsi ya kumdanganya mume au mke ni daima pia. Uzinzi haulindi familia na tena hauwalindi wanandoa dhidi ya maumivu ya hisia. 

      Maana ya Amri “Usizini” ni ulinzi kwa familia. Kwa nini familia ni muhimu sana? Kwa sababu pasipo familia uimara wa jamii hauwezekani. Kwa sababu bila familia mawasiliano ya thamani ya jamii kizazi kwa kizazi hayawezekani. Kwa maana uhusiano kati ya wazazi na watoto unawafanya kuwajibika na kukomaa zaidi. Kwa sababu bora kuliko chochote, familia inayaridhisha mahitaji ya hisia na fizikia/mwili, kuwapa watoto utoto salama na imara. Yesu anawajulisha watoto kama mfano ili tuweze kukaribisha vizuri mafundisho yake na kupata furaha kubwa. “Bila uaminifu hakuna furaha”. Familia yetu iweze kukuta njia kamili ya kuishi vizuri.

Fr Ndega



sábado, 29 de setembro de 2018

WANAFUNZI WENGINE WA YESU



Kutafakari kutoka Hes 11:25-29; Mk 9:38-43, 45, 47-48

Mungu hawabagui watu kwa maana anapenda na katika upendo hakuna ubaguzi. Matarajio yake ni watu wake wote wawe manabii, wakisikiliza neno lake na kuongea katika jina lake. Kupitia Roho wake Mtakatifu, anatuimarisha tuwatendee wote mema kulingana na mapenzi yake, akidhibitisha kwamba upendo wake hauna mpaka. Mbele ya Mungu hakuna mtu wa heshima kuliko wengine. Yeye hakubali umaarufu au ubaguzi, bali anatarajia ahadi kwa njia yake ya kufikiri na kutenda. Anatenda hivyo kwa sababu ya upendo Wake mkubwa.

Mtakatifu Yakobo anakosoa kwa nguvu watu wanaokuwa tajiri kwa njia ya udhalimu kwa kukanusha mishahara kwa wafanya kazi. Mungu anapinga hali ya udhalimu na kosa la usawa kati ya watu. Yeye ndiye tayari kutenda kwa ajili ya walio waathirika wa udhalimu na kumwomba kwa imani. Ukosoaji huu unatumika pia kwa wote ambao wajikabidhi katika mali ambayo anayo kuliko riziki ya Mungu. Mtu anapokufa hawawezi kuchukua mali chochote pamoja naye; kwa hivyo tabia ya kuongeza mali kwa nafasi yake mwenyewe haina maana.

Wanafunzi wa kwanza walijaribu kumkataza mtu fulani ya kufanya mwujiza kwa jina la Yesu kwa sababu hakuwa mmoja wao. Walifanya hivyo kwa mamlaka gani? Yesu hakukubaliana na tabia hii na kuwaambia kwamba mtu anayetenda mema kwa jina lake (Yesu) hawezi kumtendea vibaya. Kisha akiendelea kwa mafundisho yake, alisema kwamba watu wanaosaidia wafuasi wake watapokea tuzo kwa sababu ya utambulisho wake na wale waliotumiwa kwa jina lake. Yesu anawakumbusha pia kwamba mambo yote wanayofanya wale wanaomfuata yapaswa kuwaimarisha watu kumwamini Kristo. Ni lazima kuepuka Kashfa kwa sababu tabia hii inavuruga imani na kukana utambulisho wa wanaomfuata Yesu.

Tumetafakari kuhusu ugumu wa wanafunzi wa Yesu kuelewa na kuyapokea mafundisho yake. Kujaribu kumkataza mtu fulani ambaye alifanya mema kwa jina la Yesu ni ishara ya ugumu ya kumfahamu Yesu na mapendekezo yake. Maana ya kuwa mfuasi wa kweli wa Yesu siyo maneno tu, bali ni matendo mema hata kama yeyote hahudhurii kikundi. Badala ya kuwakataa wengine ambao wanatenda mema kwa jina la Yesu, wanafunzi wake wanapaswa kujikataa wenyewe. Kuwa mwanafunzi wa Yesu kunamaanisha kuishi imani iliyoonyeshwa kwa matendo. Kwa Yesu wale wanaosikiliza Neno la Mungu na kuweka vitendoni ndio mama na ndugu zake na wanafunzi wake. Hivyo yule aliyetenda mema kwa jina la Yesu anaweza kufikiriwa kama mwanafunzi wake. Mtazamo wa wanafunzi ndio tofauti na ule wa mwalimu wao kwa sababu lengo lao sio kukaribisha bado bali ubaguzi.

Kitu muhimu katika dini au imani ni matendo na siyo maneno tu. Matendo husema zaidi kuliko maneno. Wakristo wa kwanza ndio mfano halisi kwa sababu waliweza kuwavutia wengine si kwa maneno, bali kwa njia yao ya maisha. Kuhusu hao watu walisema: “Mwone kama wanavyopendana”! hali hii iliwezekana kwa sababu ya upendo wao ulionyeshwa kupitia ridhaa wao kwa wao, kushiriki pamoja, uvumilivu katika maombi pamoja na unyenyekevu wa moyo. Kuhusu hayo Sinodi ya Afrika imesema: “Sharti muhimu la kuhubiri ni ushuhuda wa maisha”. Mwanafunzi wa kweli wa Yesu hawezi kuwa na ubaguzi na kuamini kuwa watu wa kundi lake pekee ama kanisa lake ndiyo wanafunzi pekee wa Yesu na kwamba ndio hao peke yao ambao wameokolewa.

Hatuwezi kufikiri kwamba Yesu ni mali yetu. Ikiwa tunahisi karibu na Yesu, hatuwezi kuishi mbali sana na ndugu zetu, kufungwa kabisa kwa hali kandokando yetu na hata kufikiri kwamba tunakuwa na mamlaka ya kuwazuia wengine watende kwa jina la Yesu. Tuko mbele ya kosa kubwa. Tuwe macho kuhusu baadhi ya uzoefu ambao unatufungua kwa Mungu lakini unatufunga kwa wengine. Ikiwa imani yetu haituongozi kukutana na wengine na kutambua mema ambayo wanaweza kufanya imani yetu ni utenganisho. Basi, ili Mungu atufundishe kutambua mwendelezo wa kazi zake mbele ya matendo mema ya Wakristo na kusaidiana kwa wema wa wote.

Fr Ndega

sábado, 22 de setembro de 2018

YATOSHA KUWA KAMA WATOTO WADOGO



Hek 2:12.17; Yak 3: 16-4:3; Mk 9,30-37



         Andiko la kitabu cha Hekima ya Sulemani linaongea kuhusu ushuhuda muhimu wa mtu mwenye haki na upinzani wa wale ambao hawaukubali ushuhuda wake na kumtendea vibaya, hata kwa kupanga kifo chake. Hali hii inatokea kwa sababu ya uaminifu yake kwa Mungu. Mambo yote ambayo washtaki wanasema dhidi ya mwenye haki yanakuwa uthibitisho wa utambulisho wa mtu huyo aliye mwana wa Mungu naye Mungu mwenyewe atamtegemeza na kumtetea dhidi ya adui zake. Huu ndio mfano wa Kristo ambaye aliteseka sana kwa sababu ya uaminifu wake kwa mpango wa Mungu na kwa kujisalimisha kwake aliupata wokovu hata kwa wale waliomkandamiza.  

         Andiko la pili linasema kuwa hekima ambayo inasababisha kujua kamili inatoka kwa juu kwa sababu ni Mungu mwenyewe chanzo cha hekima ya kweli. Mtu anayeongozwa na hekima hii anaweza kuchagua vizuri na kuwa chombo cha amani, cha umoja na cha ushirika katika jumuiya, na kuwa tayari kusikiliza maneno ya wengine na kutenda mema kwa ajili yao.

         Injili ni mwendelezo wa tangazo la Petro kuhusu utambulisho wa Yesu na mwaliko wa Yesu mwenyewe ili wafuasi wake wamfuate katika kujisalimisha kwake ili wapate uzima. Yesu alitambua kwamba walihitaji kujua maana kamili ya utambulisho wake kama Masihi na kuyafahamu vizuri mapendekezo yake. Kwa hivyo alitumia nafasi maalum katika mahali pa faragha ili kuwafundisha. Kwa nini hakutaka watu wafahamu alipo pamoja na wanafunzi wake? Kwa sababu wazo wa Masihi ambao watu walikuwa nao ulikuwa mbali sana na utambulisho wake na kwa hivyo lilikuwa hatari kwa malezi ya wanafunzi wa Yesu.  

     Basi, bila kusukumwa na uwepo wa watu, Yesu alijiona mwenye heri kabisa ili kuwaongelea kwa uwazi kuhusu mateso, kifo na ufufuko wake, lakini walionekana mbali sana na mwalimu. Hawakuelewa tena kwa sababu walishughulika kwa mawazo na nia tofauti. Kwao ilikuwa muhimu kujadili juu ya msimamo na upendeleo kuliko kuandamana na mwalimu wao kwenye kujisalimisha. Kwa uvumilivu na kwa kutumia mtoto kama mfano, yeye aliwasaidia kufahamu ufunuo wake na masharti ya kumfuata. Yule anayeamua kumfuata Yesu anapaswa kuongoza maisha yake kulingana na mantiki tofauti na mawazo wa dunia. Ikiwa katika nafasi iliyopita Yesu aliwaomba kuyatoa maisha ili kuyaokoa, hapo aliwaomba kuwa wa mwisho na mtumishi ili kuwa wa kwanza.

          Yesu anadhihirisha utambulisho wake kama Mwana wa Adamu (mtu). Katika Agano la Kale tunakuta maneno haya katika vitabu vya nabii Danieli na Ezekieli. Kulingana na Danieli maneno haya yaongea kuhusu hali ya utukufu wa yule ambaye atakuja siku ya mwisho (Dan 7:13). Kulingana na toleo la Ezekieli maneno Mwana wa Mtu yanatumiwa na Mungu kwa uhusiano na nabii wake na kuonyesha hali ya udhaifu na kifu cha binadamu (Ezk 2:1, 3:1.25, 17:2). Basi, hii ni maana iliyotumiwa na Yesu ili kuongea kuhusu utambulisho wake kwa uhusiano na hali ya binadamu na fumbo la mateso, kifo na ufufuko wake ambalo lilisababisha ubinadamu mpya. Hivyo, tunafahamu maana ya ufundishaji wa uvumilivu  wa Yesu ili kuwasaidia wanafunzi wake walio na ujinga na udhaifu wa akili.

        Watoto wadogo wana nafasi maalum moyoni mwa Yesu. Alisema kwamba Ufalme ni wao naye mtu anayetaka kuingia katika Ufalme huu anapaswa kuwa kama watoto. Basi,  Yesu anatuongelea kwamba ni lazima mabadiliko ya mawazo na tabia ili tuweze kumfuata kwa kweli. Mfano wa watoto wadogo ni maalum kwetu kwa sababu hao wanatusaidia kutafuta muhimu zaidi ya maisha, yaani ukweli, unyenyekevu wa moyo, kuamini, n.k. Kama vile wanafunzi wa kwanza sisi pia tuko na ugumu wa kufahamu mambo yote kumhusu Yesu na mapendekezo yake, lakini tukimruhusu, yeye anaweza kufungua akili zetu na kubadilisha moyo wetu ulingane na matarajio yake. Siku ya leo yeye anatualika kwa uhusiano wa kibinafsi naye. Kupitia uhusiano huu peke yake tunaweza kuingiza utambulisho wake na kufahamu maana ya ushiriki wetu katika kazi yake ya ukombozi. Mfano wa watoto wadogo utusaidie kufahamu nia ya Yesu kuhusu maisha yetu na kukubali mapendekezo yake kwa kutumia nguvu zetu kwa ajili yake “mpaka kifo, mpaka uzima”.

Fr Ndega


É SUFICIENTE SER COMO AS CRIANÇAS



Sab 2, 12,17; Tiago 3, 16-4.3; Mc 9:30-37


      O texto do livro da sabedoria fala sobre o testemunho da pessoa justa e a oposição daqueles que não aceitam o seu testemunho e lhe tratam mal, inclusive tramando a sua morte. Isso acontece por causa de sua fidelidade a Deus. Tudo o que os adversários dizem torna-se uma confirmação da identidade daquele que sente filho de Deus e o próprio Deus virá em seu socorro, salvando-o de seus inimigos. Esta é uma imagem de Cristo que sofreu muito por causa de sua fidelidade ao plano de Deus e com o seu sacrifício trouxe a salvação até para aqueles que o oprimiam.

       O segundo texto nos fala que a sabedoria que traz o conhecimento perfeito vem do alto porque é o próprio Deus a fonte da verdadeira sabedoria. A pessoa que se deixa conduzir por essa sabedoria é capaz de fazer bem suas escolhas, tornando-se um instrumento de paz, unidade e comunhão na Comunidade; será sempre disposta a escutar os outros e a se doar pelo bem deles.

        O Evangelho continua a mensagem do domingo passado sobre a identidade de Jesus e o convite para segui-lo para obter a vida plena. Jesus percebeu que os seus discípulos precisavam conhecer o verdadeiro significado de sua identidade como Messias de Deus e entender bem suas propostas; Por esta razão, ele decidiu leva-los para um lugar longe do povo para ensiná-los. Jesus deseja estar a sós com os seus discípulos. Por que ele não queria que as pessoas soubessem onde ele estava com seus discípulos? Porque a ideia de Messias que as pessoas tinham era longe daquilo que era sua identidade e isso era perigoso para a formação de seus discípulos.

       Finalmente, sem a presença da multidão, Jesus se sente mais livre para falar a eles com a sinceridade do seu coração sobre o mistério do seu sofrimento, morte e ressurreição, mas eles pareciam distante do mestre. Eles não entenderam porque não estavam atentos; tinham outras motivações e pensamentos. Era mais importante para eles discutir posições e privilégios do que acompanhar o mestre para a total entrega de si. Pacientemente e pegando uma criança como exemplo, Jesus os ajudou a compreender a sua revelação e as condições para segui-lo. Quem decide seguir Jesus deve conduzir a sua vida segundo uma lógica diferente da mentalidade deste mundo. Se na última vez, ele disse que é doando a vida que se pode salvá-la, desta vez diz que é preciso ser o último e servo dos demais para poder ser o primeiro.

         Esta realidade revela a identidade do Mestre Jesus que se fez servo por amor. Ele se revela como Filho do homem por causa de seu envolvimento com a realidade humana. No antigo testamento encontramos esta expressão nos livros de Daniel e Ezequiel. De acordo com Daniel, este "Filho do homem" refere-se à glória daquele que virá no fim dos tempos (Dan 7:13). De acordo com a versão de Ezequiel, "filho do homem" é o título usado por Deus no relacionamento com seu profeta e expressa a condição frágil e mortal do ser humano (Ezek. 2,1, 3:1.25, 17,2). Assim, este é o sentido usado por Jesus para falar sobre sua identificação com a condição humana e o mistério da sua paixão, morte e ressurreição a partir do qual surge uma nova humanidade. Assim, entendemos a razão da pedagogia o paciente e criativa de Jesus em relação aos seus discípulos, "duros de coração lentos para crer".

        As crianças têm um lugar especial no coração de Jesus. Ele disse que o Reino de Deus pertence a eles e aqueles que querem entrar neste reino devem tornar-se como as crianças. Então, Jesus nos fala sobre a necessidade de mudança de mentalidade e atitude para que possamos segui-lo verdadeiramente. O exemplo das crianças é especial para nós porque nos ajudam a buscar o que é mais importante na vida, isto é, a verdade, a simplicidade de coração, a confiança, etc. Como os primeiros discípulos, nós também não compreendemos tudo sobre Jesus e suas propostas, mas se lhe damos permissão, ele pode abrir nossas mentes e transformar nossos corações para que sejam de acordo com suas expectativas sobre nós. Jesus nos chama para uma relação pessoal com ele e é somente através de uma relação assim que podemos assimilar sua pessoa e entender o que ele quer de nós, isto é, o sentido de nossa participação como seus colaboradores em sua missão Redentora. O exemplo dos "pequeninos" nos ajude a entender a intenção de Jesus sobre a nossa vida e a acolher a sua proposta, usando todas as nossas energias pela sua causa, "até à morte, até à vida".

Fr Ndega


BASTA ESSERE COME I BAMBINI



Riflessione su Sap 2, 12.17; Giac. 3, 16-4,3; Mc 9,30-37


       Il brano della Sapienza parla sulla testimonianza del giusto e della opposizione di coloro che non accolgono la sua testimonianza e lo trattano in modo cattivo, anche tramando la sua morte. Questo succede a causa della sua fedeltà a Dio. Tutto quello che dicono gli avversari diventa una conferma dell’identità di colui che si sente figlio di Dio e il proprio Dio verrà in suo soccorso, salvandolo dai suoi nemici. Questa è una immagine di Cristo che ha sofferto molto a causa della sua fedeltà al progetto di Dio e con il suo sacrificio ha portato salvezza anche per coloro che lo opprimevano.

        Il secondo testo ci comunica che la sapienza che porta la perfetta conoscenza viene dall’alto perché è Dio stesso la sorgente della vera sapienza. La persona che si lascia condurre da questa sapienza può fare bene le sue scelte, diventando strumento di pace, di unità e comunione nella comunità; sarà sempre disposta ad ascoltare gli altri e a donare se stessa per il loro bene.

     Il vangelo continua il messaggio della volta scorsa sull’identità di Gesù e l’invito a seguirlo per ottenere vita piena. Gesù ha percepito che i suoi avevano bisogno di conoscere il senso vero della sua identità come Messia di Dio e capire bene le sue proposte; per questo ha deciso di usare una opportunità speciale in un posto in disparte per insegnare loro. Perché non ha voluto che la gente sapesse dove era lui con i suoi? Perché l’idea di messia che la gente aveva era lontano dalla sua identità e per questo era anche pericolosa per la formazione dei suoi discepoli.

        Senza la presenza della folla, Gesù si sente più libero per parlare ai suoi con sincerità sulla sua sofferenza, morte e risurrezione, ma loro sembrano lontani dal loro maestro. Non capivano perché non erano attenti, avevano altre motivazione e pensieri. Per loro era più importante discutere circa posizioni e privilegi che accompagnare il maestro verso la totale consegna di sé. Con pazienza e prendendo un bambino come esempio, Gesù li ha aiutati a capire la sua rivelazione e le condizioni per seguirlo. Chi decide di seguire Gesù deve condurre la sua vita secondo una logica diversa dalla mentalità di questo mondo. Se nella volta scorsa, egli ha detto che è donando la vita che si può salvarla, questa volta dice che bisogna essere l’ultimo e servo degli altri per essere il primo.

        Questa realtà rivela l’identità propria del Maestro Gesù che si è fatto servo per amore. Lui si rivela come Figlio dell’uomo a causa del suo coinvolgimento con questa realtà. Nel Vecchio Testamento troviamo questa espressione nei libri di Daniele e di Ezechiele. Secondo Daniele questo “Figlio dell’uomo” riferisce alla gloria di colui che arriverà alla fine dei tempi (Dan 7:13). Secondo la versione di Ezechiele, “Figlio dell’uomo” è il titolo usato da Dio nei confronti del suo profeta ed esprime la condizione fragile e mortale dell’essere umano (Ez. 2,1, 3:1.25, 17,2). Quindi, questo è il senso usato da Gesù per parlare della sua identificazione con la condizione umana e il mistero della passione, morte e risurrezione da cui sorge una nuova umanità. Così, possiamo capire il senso della pedagogia paziente e creativa di Gesù nei confronti dei suoi discepoli, “stolti e lenti di cuore”.

       I bambini hanno un posto speciale nel cuore di Gesù. Egli ha detto che il Regno di Dio appartiene a loro e chi vuole entrare in questo regno deve diventare come loro. Quindi, Gesù ci parla sulla necessità di cambiamento della mentalità e atteggiamento affinché possiamo seguirlo veramente. L’esempio dei bambini è speciale per noi perché loro ci aiutano a cercare ciò che è più importante nella vita, cioè, la verità, la semplicità di cuore, il fidarsi, ecc. Come i primi discepoli anche noi non riusciamo a capire tutto su Gesù e le sue proposte, ma se gli diamo il permesso, egli può aprire la nostra mente e cambiare il nostro cuore perché sia secondo le sue aspettative su di noi. Gesù ci chiama a una relazione personale con lui ed è solo all’interno di una relazione che possiamo assimilare la sua persona e capire cosa vuole da noi, cioè, il senso della nostra partecipazione come suoi collaboratori nella sua opera redentrice. L’esempio dei “piccoli” ci aiuti a capire l’intenzione di Gesù sulla nostra vita e ad accettare le sue proposte, spendendo tutte le nostre energie a causa sua, “fino alla morte, fino alla vita”.

Fr Ndega

sábado, 15 de setembro de 2018

UAMINIFU WA MUNGU NI NGUVU YETU


Kutafakari kuhusu Isa 50:5-9; Yak 2,14-18 Mk 8:27-35


     Mtumishi wa Bwana anajiona kuimarishwa kwa sababu ya uhakika wa upendo na utunzaji wa Mungu daima maishani mwake. Uhakika huu unamfanya imara mbele ya mateso mengi. Yule ambaye anamtumainia Bwana habaki kuchanganyikiwa na mwenye udanganyifu kwa sababu “uaminifu wa Bwana ndio nguvu yetu”. Mtakatifu Yakobo anawaomba Wakristo wawe walio halisi katika njia ya kuamini. Imani inayoonyeshwa kwa maneno peke yake siyo kweli. “Maneno yatoweka hata ikiwa yanaonekana yawe na imani. Matendo yanaiweka halisi kwa kuifanya iwe iko na sasisha”. Basi, ndiyo matendo mema ambayo yadhihirisha ukweli wa imani yetu. Madre Teresa wa Kaukuta alikuwa na haya ya kusema: “Kila tendo la upendo linalofanyika kwa moyo linaweka halisi imani kwa kumkaribia Mungu”.

      Yesu alikuwa anatembea pamoja na wanafunzi wake. Walipofika karibu na Kaisaria Filipi aliwauliza maswali kuhusu utambulisho wake kulingana na mtazamo wa watu. Majibu yalikuwa ishara ya kwamba mawazo kuhusu Yesu hayakuwa wazi sana kwa upande wa watu. Ingawa hayakuwa wazi kwa watu, ni lazima kuwa tofauti kwa mitume kumi na wawili, kwa sababu kwa Yesu haikuwa muhimu sana yale ambayo watu walifikiri, bali imani na kukiri kwa wafuasi wake. Petro alidhihirisha yale ambayo wanafunzi wengine kumi na mmoja walijua pia: Yesu ni Masiya wa Mungu. Lakini hawakuweza kuitangaza habari hii kwa sababu ya kosa la maana kamili. Yesu alitambua kwamba wafuasi wake walihitaji kujua kwa kina maana ya utume wake kama Masiha na masharti kwa kumfuata kwa kweli.

        Mawazo ya wafuasi wa Yesu kuhusu Masiya yalifuata matarajio ya Wayahudi wengine, yaani, Masiya wa kisiasa atakayetumia nguvu zake za kimungu ili kuwakomboa Wayahudi toka ukoloni wa Warumi. Bila shaka Yesu alikataa mawazo hayo kwa kuonyesha njia tofauti ya kutimiza mpango wa Mungu, yaani kupitia mateso, kifo na kufufuka. Njia aliyochagua Yesu ni ile ya mtumishi wa Bwana wa nabii Isaya. Utambulisho wa mtumishi huyo ni kuwa makini kwa sauti ya Mungu ili aweze kufanya mapenzi yake kwa kutumikia kabisa. Kwa kufanya mapenzi ya Mungu mtumishi huyo alipaswa kuteseka na kufa, lakini alisimama upande wa Mungu ambaye alimsaidia akimfanya mshindi. Itikio la Petro lilidhihirisha upinzani dhidi ya njia ya maisha Yesu aliyochagua ili atimize mapenzi ya Mungu. Uamuzi wa Yesu ulikuwa katika ushirika na Baba yake na upinzani dhidi ya njia hii ni upinzani dhidi ya mapenzi ya Mungu.

        Wanafunzi wa kwanza walihitaji mwendo wa muda mrefu ili kujifunza kumhusu Yesu na kuyafahamu mapendekezo yake sawasawa. Yesu alimkemea Petro lakini alimwalika afuate mtazamo wa Mungu ili awe mwanafunzi wa kweli. Kidogo kidogo wote walitambua kwamba kwa kujitoa kama Yesu alivyo, walipaswa kuzifuata hatua tatu, yaani, kujikana wenyewe, kuichukwa misalaba yao na kumfuata Yesu. Kwa maneno mengine, walipaswa kuyabadilisha maisha yao kabisa. Wale ambao hukutana na Yesu hawakubaki walivyo na hawawezi kumwomba Yesu atende kulingana na mapendekezo yao. Mwendo wapaswa kuwa tofauti. Kwa kumfuata Yesu kweli tunapaswa kupatikana kwa mambo yote kwa ajili ya ufalme wa Mungu kwa kuyaingiza mapendekezo ya Yesu. Tunapaswa kufananisha maisha yetu kulingana na njia ya Yesu ya kuishi  na kuchukua msalaba kama yeye alivyo.


     Injili siku ya leo inatusaidia kutafakari kuhusu njia ambayo tumechagua ili kumfuata Yesu. Je, hii ni njia ya kweli? Tunatambua kwamba Kumfuata Yesu hakuuleti upendeleo au hadhi, bali mateso na kujisalimisha kwa ajili ya injili. Basi, yeyote ambaye anataka kuishi kwa shwari na bila ahadi hawezi kumfuata Yesu. Yeyote ambaye anatamani kumfuata Kristo bila msalaba hatamfuata Kristo kwa kweli kamwe. Kupitia mambo hayo tunaweza kujiuliza maswali: Je, Kristo gani tumemfuata? Mawazo au kitu gani tunahitaji kujinyima bado ili tuweze kumfuata Yesu kikamilifu? Maisha yetu ya kawaida ni ishara ya kwamba tumekuta hazina yetu ya kweli? Tuishi wito wetu wa wanafunzi wa Yesu kwa shauku na furaha kwa sababu Mungu ndiye mwaminifu na kuwa tayari daima kutusaidia hasa wakati tuko na ugumu wa kubeba msalaba wetu. Tumwaminie yeye kwa sababu uaminifu wake ni nguvu yetu.

Fr Ndega